255 Young Rich Team

255 Young Rich Team KUHUSU LIFE CLINIC
Life clinic ni huduma inayotolewa na kampuni ya KICHUCHU CO.

LTD ambayo inalenga kukuza biashara ndogo na ujasiliamali hapa nchini Tanzania kwa kutoa misukumo,taarifa za kibiashara, na mitandao na pia kuwezesha wafanya biashara wadogo kuanza,kukua na kutanuka. Huduma hii pia inatoa hamasa na motisha kwa biashara ndogo na za kati kuweza kufanya biashara zao kwa ushindani katika masoko.Huduma hii sio ya kidini wala haifungamani na upande wowote wa kisiasa kwa

ni maendeleo ni kwa wote. IMANI YETU
Sisi tunaamini kwamba matatizo yanayozuia maendeleo ya Wajasiriamali Tanzania ni pamoja na ukosefu wa mitaji na elimu ya biashara,Elimu ya maisha,Elimu ya kiafya,Elimu ya Uongozi..hivyo lengo letu ni kuhakikisha tunatoa elimu hizo na jamii yetu iweze kupata maendeleo na mafanikio zaidi hususani kwa vijana wa kitanzania

Kwa mawasiliano zaidi au kuweka matangazo,tafadhali wasiliana nasi kupitia:

kichuchu company limited
phone: +255768566054
email:[email protected]
MWANZA - TANZANIA

24/01/2017

Anaitwa Madam Deborah Mallaba Mkurugenzi mtendaji wa taasisi ya AmitzMwanza anaamini NDOTO za mafanikio hutengenezwa kuanzia chini.
Gonga Like umwambie wewe unasemaje

FURSA YA MAFANIKIO MKOA WA MWANZA 2017 HII HAPA NJOONI TUJIFUNZA NAMNA AMBAVYO KILIMO BIASHARA KINALIPA
24/01/2017

FURSA YA MAFANIKIO MKOA WA MWANZA 2017 HII HAPA NJOONI TUJIFUNZA NAMNA AMBAVYO KILIMO BIASHARA KINALIPA

AmitzMwanza
MBOGA HADI MLANGONI
AmitzMwanza ni kifupi cha taasisi ya AGRIBUSINESS MEDIA INITIATIVE MWANZA inayojihusisha na uhamasishaji na kilimo biashara pamoja na uibuaji na utoaji elimu kwa watu za kijasiliamali kwa kupitia mradi wake wa ulimaji mbogamboga jijini mwanza sasa unaweza kuagiza nasi tuka kuletea popote ulipo hapa jijini mwanza
pasipo gharama yeyote ya usafirishaji.
Pia tunatoa mafunzo kwa vikundi au mtu mmoja mmoja juu ya namna ya kukabiliana na umasikini kwa kupitia kilimo bishara

Wasiliana moja kwa moja na mkurugenzi mtendaji kwa 0754996613

05/10/2016

Fanya kulike kwa mafanikio ya kweli

05/10/2016

Kuna ngazi 4 za uwezo (competency)

• Unconscious incompetency – Hujui kwamba hujui….
• Conscious Incompetency – Unajua kwamba hujui
• Conscious competency – Unajua kwamba unajua
• Unconscious competency – Unafanya bila kujua. Hujui k**a unajua

Asilimia kubwa ya watu waliofanikiwa ni Unconscious competent (wana uwezo ambao wenyewe hawaujui). Tatizo linakuja pale wanapowafundisha watu jinsi walivyofika hapo walipo, wanachowafundisha watu unakuta mara nyingi si hicho kilichowafikisha hapo japo wao wanadhani kwamba wamefikia hapo kwa sababu ya hivyo wanavyofundisha. Tatizo ni kwamba wao wenyewe hawajui maana ukiwa katika level ya Unconscious competency katika jambo fulani unakua hujui hata huwa unalifanyaje. Secret code ya mafanikio haipo katika conscious mind, bali ipo katika unconscious mind ndiyo maana hata hao waliofanikiwa inakua ngumu wao kujua k**a hiyo secret code k**a ipo.

01/08/2016

Siku zote katika mfumo wako wa maisha tambua k**a huna watu wanaokuchukia au kukuletea fitina basi tambua hadi hapo ulipo hakuna kubwa ulilowahi kulifanya wakaliona..ila ukiona watu wanakufatilia tambua sasa umekuwa na safari ya mafanikio inakunyemelea lakufanya ni kuanza kuzitumia changamoto hizo kwa kuzifanya ndio chachu kubwa ya mafanikio badilika

21/07/2016

Chochote unachokifanya kifanye vizuri.kifanye vizuri il watu wakiona unakifanya watamani kurudi tena wakuone ukifanya tena na watamani kuwaleta wengine wawaonyeshe jinsi unavyofanya vizuri kile unachokifanya

08/07/2016

JINSI YA KUBAKI KUWA MASIKINI.

1. Kamwe usiamke mapema, endelea kulala na kujinyosha mpaka pale njaa itakapokuuma.

2. Kamwe usipange jinsi ya kutumia pesa zako, wewe zitumie tu pale unapozipata. Na zikiisha kaa chini na jifikirie umezitumiaje.

3. Kamwe usifikiri juu ya ku 'save' pesa zako, subiri mpaka uwe nazo nyingi ndio uanze ku 'save', utasave vipi pesa zako wakati unazo kidogo? Wanaokuambia usevu pesa hawakutakii mema katika matumizi yako.

4. Kamwe usijiingize katika biashara ambazo huwa mnaziita 'za wasiosoma' wewe ni mhitimu wa chuo kikuu ulie soma bhana utafanyaje biashara ya viazi? Utauzaje duka? Utauzaje viatu vya mitumba? Hizo ni biashara za wasioenda shule. Wewe unapaswa ukae ofisini upigwe na kiyoyozi.

5. Kamwe usifikiri kuanzisha biashara mpaka pale Malaika atakaposhuka toka mbinguni kukuletea mtaji wa kuanzia biashara. Watakuambiaje uwekeze wakati hujapata hata Milioni? Hata k**a wafanyabiashara wengi k**a kina bakheresa walianza kuuza mgahawa, wewe ni smart, unatakiwa uanze na mamilioni katika biashara zako.

6. Lalamika kuhusu kila kitu, isipokuwa usilalamike kuhusu uvivu wako na attitude yako. Ilaumu serikali ya Magufuli, zilaumu benki zilizogoma kukukopesha fedha, zilaumu kampuni mbalimbali ambazo zimekutosa kwenye ajira. Wote hao wana roho mbaya hawataki kukufanya uwe tajiri!

7. Tumia pesa nyingi tofauti na unachokipata. Kufanikisha hili nunua bidhaa za kutumia kwa mkopo, azima pesa kwa washkaji nunua kitanda cha Milioni moja, nunua Brand new LG flat screen, pendezesha kwako. Kopa pesa benki nunua Verossa, watoto wa mjini wakukome.

8. Shindana katika kuvaa. Hakikisha unavaa kila aina ya fashion mpya ya nguo. Nunua kila aina ya simu mpya inayotoka, k**a ulinunua sumsung galaxy S6 kwa milioni moja, uza hata laki sita halaf ongezea hela ukanunue sumsung galaxy S7. Zimetengenezwa kwa ajili yetu bhana.

8. Ukishindwa kununua gari mpya, nunua gari ya mtumba ambayo gharama zake za kulihudumia ni mara mbili ya mshahara unaoupata, au gari linalokaa muda mrefu gereji kuliko barabarani.

9. Wape wanao kila wanachokitaka kwa kuwa wewe ni mzazi bora, hawatakiwi kuhangaika wala kufundishwa utu na thamani ya pesa, usiwafundishe juu ya kutunza na kuheshimu fedha. Usiwafuatilie kabisa katika masomo yao.

Waache wakue wakiwa wavivu na waje kuwa masikini kuhakikisha kuwa hawawezi kukusaidia pale utakapozeeka.

10. Tembelea viwanja vyote vya bata, na uzuri wamiliki wa maeneo ya starehe wanatujali yaani wanafungua maeneo mapya kila siku, tembelea yote. Kula bata kula bata.

Na ukishakuhakikisha kwamba unatekeleza hayo yote, kaa chini na utafakari kuwa siku zote fainali nzuri huchezwa uzeeni!

Ponda raha kufa kwaja!

I DO NOT CARE

05/07/2016

FURSA FURSA FURSA!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!INUKA BADILIKA COMING SOON
Baada ya Mafanikio tuliyoweza kuyapata, vilevile na maombi toka kwa wadau mbali mbali walioweza kufanikiwa kupitia elimu ya kilimo biashara, AmitzMwanza toka jijini mwanza kwa kushirikiana na Kichuchu MEDIA watakuwa na kampeni kabambe kwa jina la INUKA BADILIKA yenye kauli mbiu ya MAISHA NIKUBADILIKA,KUBADILIKA NI KUISHI KATIKA NJIA SAHIHI itakayotoa mafunzo ya BIASHARA,MIKOPO,MITAJI na mengine kibao lengo kuu likiwa ni kupambana na umasikini kwa kuondoa dhana ya maisha tegemezi mfano AJIRA nakukimbilia dhana ya KUJIAJIRI MWENYEWE HIVI KARIBUNI HAPA JIJINI MWANZA HIVI KARIBUNI .
Mafunzo yatakuwa ya nadharia na vitendo. Mafunzo yatahusu:
1. MBINU BORA ZA BIASHARA,
2. FAIDA YA KUJIAJIRI
3. JINSI YA KUPATA MITAJI.
4. ELIMU YAKUJITAMBUA.
5.JINSI YA KUPATA WAZO BORA LA BIASHARA NASIO BORA WAZO
6.JINSI YA KUUZA BIDHAA ZAKO
Walengwa: VIJANA WOTE WENYE HAMASA YA KUPATA MAFANIKIO KWA NJIA SAHIHI,,NAWENYE MTAZAMO CHANYA JUU YA MAFANIKIO YAO.
Pia washiriki wataweza KUPATA NAFASI YA KUTAFTIWA MASOKO KUTOKANA NA BIDHAA ZAO KWA HUAKIKA ZAIDI PASIPO SHAKA PAMOJA NA KUKUTANISHWA NA WADAU MBALIMBALI WALIOWEZA KUFANIKIWA PASIPO KUAJIRIWA.
KWAMASILIANO ZAIDI JUU YA KAMPENI HII WASILIANA NASI KUPITIA:
+255754996613/+255768566054
KAA MKAO WA KULA
INUKA BADILIKA

22/01/2016

FURSA
je utawezaje kutambua fursa na kuweza kuanzisha biashara katika mazingira yako? Bila shaka hili swali watu wengi wanaotamani kumiliki biashara zao binafsi wamekuwa wakijiuliza mara kwa mara pasipo kutilia msisitizo katika maisha yao. Unaweza kufikiri mambo mengi sana kuhusu namna ya kuwa na biashara yako binafsi lakini kutokuwa na nia madhubuti ni sababu kuu inayokufanya usite na hata kupoteza utayari wako wa kutaka kumiliki biashara yako binafsi.
Kwanza kabisa ni muhimu ujue FURSA maanake ni nini hasa, kwa ufafanuzi rahisi FURSA ni uwezo wa mtu kutambua nafasi/bahati yenye manufaa kwake kulingana na kile alichoazimia kupata au kufanikiwa. Fursa zipo tele ila huwezi kuona fursa ikiwa hujaazimia kufanya lolote hata k**a utapata nafasi ya kutumia fursa yenyewe au ikiwa huna malengo yeyote yale.
JE UTAWEZAJE KUONA AU KUTAMBUA FURSA?
Utaweza kuona fursa ikiwa tayari ulishakuwa na malengo ya kufanya biashara yenyewe. Hapa ni kwamba kuwa na mpango wa kufanya biashara kabla kuanzisha biashara yenyewe ndio njia pekee ya kuweza kuona fursa itakayojitokeza mbele yako kwakuwa tayari ulishakuwa na mawazo juu ya fursa hiyo.
Mfano: Katika mtaa unaoishi kuna shughuli nyingi za ujenzi zinaendelea. Kutokana na shida ya upatikanaji wa vifaa na vitu vingine vya ujenzi k**a simenti, mbao, tiles, mabati nakadhalika.
Kwasababu ulishakuwa na wazo la biashara ya Hardware Shop ama kwa kusikia au kuona kwa mtu mwingine ambaye tayari anafanya biashara hiyo ya Hardware Shop labda mahali pengine. Ni rahisi kwako kuona fursa ya kuanzisha Hardware Shop yako mwenyewe katika mtaa wako kwa kuwa tayari ulishakuwa na wazo hilo.
Hatimaye utakavyoweza kuona fursa utaweza kuamua kuwasogezea huduma watu wa mtaani kwako kwa kufungua duka kubwa la Vifaa Vya Ujenzi (Hardware Enterprise). Pia kwakuwa mahitaji ya vifaa vya
ujenzi ni makubwa, unapanga bei nakuuza bidhaa zako kwa bei poa na watu wa mtaani kwako watamiminika kununua bidhaa zako zilizo bora kabisa.
Tumia hizi mbinu 3zikusaidie kutambua fursa.
1. Tafakari biashara yoyote ile unayopenda kufanya kwa kuandika katika karatasi. (Tafakari bila kufikiria ugumu wa kuanzisha biashara yenyewe)
2. Kati ya biashara ulizoorodhesha, fikiri katika maeneo yako ni biashara gani ambayo bado haijafika katika eneo lako na ina mahitaji makubwa. Andika chini kwenye karatasi na orodhesha mambo muhimu yanayohitajika kuanzisha biashara yenyewe.
3. Kisha andika mambo yote utakayohitaji kufanikisha kuanzisha biashara hiyo mfano: Kutathmini kiasi cha mtaji unachohitaji, mfanyakazi au idadi ya wafanyakazi wa kukusaidia nakadhalika.
Zingatia hayo mambo hayo matatu hakika utafungua maono yako na kuweza kuona fursa, pia Jambo muhimu zaidi katika kukuletea mafanikio ni KUAMINI kuwa unaweza kupata mafanikio makubwa kupitia
mawazo na mipango yako binafsi na kujiajiri mwenyewe. Kikubwa jipange kwa kutumia hizo mbinu 3, ukishakuwa tayari usiogope kuchukua hatua nyingine ya kutafuta mtaji wa kukuwezesha kufungua biashara yako na hakika ukithubutu kujaribu utafanikiwa. 0768566054

ANZA SASA KUTUMIA KIPAJI CHAKO(SANAA), ACHA KUWA MTUMWA WA SANAA.Utumwa kwa tafsiri nyepesi ni ile hali ya mtu kufanyish...
19/01/2016

ANZA SASA KUTUMIA KIPAJI CHAKO(SANAA), ACHA KUWA MTUMWA WA SANAA.
Utumwa kwa tafsiri nyepesi ni ile hali ya mtu kufanyishwa jambo pasipo hiari ya muhusika kwa lazima. Kwa upande wa sanaa,utumwa wa kisanaa ni ile hali ya msanii kutumikishwa mambo mbalimbali pasipo faida yeyote kwako,mfano kupangiwa ghrama za kazi,utendaji au maisha kutoka kwa mdhamini wake.
Wengi wanasema sanaa ni ngumu, hadi mtu kuweza kutimiza malengo ya kisanaa. lakini swali muhimu hapa kuna mtu alishawahi jiuliza kuwa yeye ana itawala vipi sanaa yake? Iwe ya filamu,mziki,uandishi au vichekesho?au zaidi anakuwa mtumwa wa sanaa kwa kutumiwa na watu wengine kupitia kazi zake?Siku moja nikiwa naongea na badhi ya vijana wenzangu nikawauliza hivi inakuwaje watu wengi wana vipaji lakin hawa endelei? Jibu walilonipa ni kuwa “watu wengi wamekuwa wakidhulumiwa na kunyanyaswa ndani ya sanaa na watu binafsi kwa maslahi yao”. Lakini nilipo wauliza je,hawa wasanii wana fahamu njia kamilifu itakayo wasaidia kuweza kutumia kipaji chako(sanaa) vizuri na kuondokana na utumwa wa kisanaa? niliendelea kuuliza je mara ngapi wasanii wanapata nafasi nzuri lakini wanashindwa na kubaki k**a watumwa wa kisanaa kwa maslahi ya watu wengine,mfano wadhamini na wasanii wakubwa?Hakuna alienipa jibu.tunapata muda wa kulalamika juu ya hali za wasanii hapa nchini lakini tunashindwa kutambua mambo muhimu ambayo mtu yeyote mwenye kipaji anaweza kuyatumia kutimiza ndoto zake na kuachana na utumwa wa kisanaa. lolote. Sanaa ni hazina ambayo ikitumika vizuri huleta mafanikio kwa mhusika
Kuna sababu amabazo hupelekea wasanii/wenye vipaji wengi kushindwa kutumia sanaa/vipaji vyao vema na kubaki kuwa watumwa wa sanaa nazo ni:
Kutokuwa na malengo;Ni ngumu sana kufanikisha jambo lolote lile endapo k**a hujaweka malengo ambayo yanaeleweka mfano ni vip utaendesha na kusimamia sanaa/kipaji chako,lini,wapi utaanza kukitumia kipaji chako vizuri nk
Kutokuwa na mpangilio; k**a ilivyo kutokuwa na malengo pia jambo lisilokuwa na mpangalio unaoleweka,mtiririko mzima wa hilo jambo,dalili hizo hupelekea jambo kuchukua muda ili kuweza kufanikiwa au kutofanikiwa kabisa. Mfano wasanii wengi hapa nchini hufanya kazi zao pasi na mtiririko mzuri wa kisanaa kwa kigezo eti msanii lazima uwe kiraka.
Uwezo wa kushindwa kusema hapana;Wote tunapenda kusaidia wengine ili wafanikiwe k**a sisi tunavyohitaji msaada kutoka kwa wengine lakini wakati mwingine mtu utakuta malipo anayolipwa msanii ni madogo kulingana na umuhimu wake na faida atakayo enda kumpatia mdhamini wake,lakini yeye hukubali tu, kushindwa kusema hapana kwa kigezo cha umaskin au shida ya kuwa maarufu.na mtu huyo(mdamini/mdau) wa sanaa akijua kwa kweli jambo hilo atakutumia ipasavyo na kukufanya uwe mtumwa wa kisanaa. Hapa lakufanya nikuwa na msimamo binafsi juu ya kazi unayokwenda kufanya ila isiwe garama ya juu kwani unaweza kukosa wadhami,iwe ya kuridhisha.
Kuingiliana mambo;mara kadhaa tumekuwa katikati ya jambo fulani ghafla kitu fulani ambacho nacho ni muhimu kikaja mfano msanii ukapigiwa simu kuwa kuna kazi inabidi ukafanye muda huo yenye dau nono nawe ukaiacha uliyo kuwa ukifanya na kukimbilia ile. Kamwe hilo si jambo jema kwa msanii kwan lita kupunguzia uaminifu nakukufanya uendelee kuwa mtumwa wa sanaa yako daima.
Namna ya kufanya ili uwe mshindi katika kutumia muda vema:
to be continues........

27/12/2015

vitu vya kutambua baada ya kuwa mfanyabiashara au mjasiriamali
biashara au ujasiriamali ni ndoto za watu wengi lakini asilimia kubwa husahau vikwazo na vizingiti ambavyo hutokea kabla na baada ya kuwa mjasiriamali au mfanyabiashara

kuna vitu na mambo mengi ambayo unatakiwa kuyafata ili ufanikiwe katika kila hatua ya biashara au ujasiriamali wako baadhi ya vitu hivyo ni pamoja na

Baada ya kuwa mjasiriamali au mfanyabiashara

1. Biashara ni ushindani, na nafasi ya makosa

Moja kati ya vitu ambavyo unatakiwa kutambua ni biashara ni ushindani ili biashara
Iendelee lazima ipate ushindani wa kutosha ndipo biashara itakuwa biashara ila k**a
Hakuna ushindani hautakuwa unafanya biashara bali unatoa huduma,mfano kwa kampuni k**a
Tanesco wao hawafanyi biashara wanatoa huduma kwa sababu hawana mshindani wa moja moja , katika Biashara kuna aina tatu za washindani kuna washindani wa moja kwa moja ( hawa ni wale ambao wanafanya biashara ka ma ya kwako), wasio wa moja kwa moja ( hawa ni wale ambao wanafanya biashara mbadala wa biashara yako) na wa tatu ni dhahania ( hawa ni wale ambao hawajaanza kutoa huduma au kufanya biashara lakini wana wazo la kufanya biashara k**a yako), kwa Tanesko wao hawana mshindani wa moja kwa moja ila wana washindani wasio wa moja kwa moja k**a wauza jenereta na umeme wa jua. Hivyo katika biashara ushindani ni kitu muhimu ili uendelee unapokuwa mfanyabiashara au mjasiriamali lazima utegemee ushindani na kila siku angalia vitu viwili kwa makini katika biashara yako wateja wako pamoja na washindani wako .

Kitu kingine cha kuongezea hapo ni pia ukiwa mfanyabiashara unatakiwa utambue biashara ni nafasi ya makosa, mshindani wako muda wote anaangalia unamapungufu gani ili atumie mapungufu yako kujiongezea wateja hivyo unatakiwa kuwa makini kuangalia mapungufu ya washindani wako na pia kuangalia maamuzi yako,mbinu unazotumia kuongeza wateja na aina ya ujumbe unaoufikisha kwa jamii.asilimia kubwa ya washindani hutumia vitu hivyo kuona mapungufu yako.

2. Muonekano wako unaathiri biashara yako

Ukiwa k**a mfanyabiashara au mjasiriamali muonekano wako unanafasi kubwa sana katika biashara yako na muonekano huu unajumulisha ,mavazi, matendo na uwezo wako wa kufikiri mara nyingi akija mtu ambae anahitaji kukudadisi na kujua unafanye biashara yako ni lazima atakuuliza kuhusu matatizo mnayoyapata na njia mnazotumia kuyatatua hii yote ni kuangalia ni kiasi gani unauwezo wa kukabiliana na matatizo na je ni mtu wa aina gani anaeongea nae , hivyo mara zote angalia sana muonekano wako kuanzia kwenye familia yako hadi kwenye jamii yako ni jambo la kawaida kusikia " ooh fulani ameanzisha biashara fulani " halafu jibu linatoka " mlevi huyo haiwezi kudumu " hii inamaanisha alieanzisha hiyo biashara muonekano wake na jamii inamchukulia k**a mlevi na tayari muonekano huo unaunganishwa moja moja kwenye biashara yake japo biashara sio yeye ila muonekano umemtengenezea. Hakikisha muonekano wako unashabihiana na biashara yako na nafasi uliyonayo katika jamii.

3.Maneno yako ndio biashara yako

Kitu kingine kinachosimamia biashara ni kauli, au maneno yako mwenyewe, ukiwa k**a mfanyabiashara unatakiwa mdomo wako uwe na nidhamu na uwezo wa kutamka yaliyo ya staha na pia unatakiwa uzijue lugha za biashara ili kutofautisha majibu unayoyatoa nyumbani sio sawa na unapokutana na mteja ,mfanyabiashara au mjasiriamali mwenzako .

4.Sheria za pesa

Ukiwa k**a mfanyabiashara au mjasiriamali unatakiwa uzijue na sheria za pesa pia , sheria kuu ya pesa ni matumizi hivyo pesa sio ya kutunzwa ili ikuzalishie nyingine pesa ni ya kutumiwa ili ikuzalishie nyingine, watu wengi huwa wanaamini mtu mwenye pesa nyingi ni yule ambaye akaunti yake inasoma fedha nyingi kwa nji za wenzetu na watu waliondelea sawa lakini kwa wafanyabiashara wadogo na wafanyakazi ni uongo, mfano : utakuta mtu ametunza mshahara wake kachanganya na fedha zake za pembeni akihisi ni hela ya kuweza kuongea na mtu na ukamwambia basi utasikia sasa hivi nnahela k**a millioni 10,20,50,90. Lakini ile fedha ukiingalia kwa umakini sio ya kwake mimi ninaamini kwamba lile karatasi au sarafu unayoishika huwa ni karatasi na sarafu za kuwakilisha thamani tu na ukiwa nalo sio la kwako mfano: umelipwa mshahara millioni 10 ukitoka tu kuwepa tayari inakuwa imeisha hata kabla haujaitoa mikononi mwako sababu hiyo pesa tayari inamahitaji yake. Kuna siri moja iko hivi wewe unapofanya kazi ili ulipwe unakuwa unaifanyia mipango hela ambayo atakupa bosi wako lakini pia kuna mtu mwingine ambae pia anakusubiri ukishaichukua hiyo pesa umpelekee wewe ni bosi wake na yeye pia kuna mwingine ambae akishaichukua hiyo fedha ni lazima amplekee ili aishi huo ndio mzunguko na sheria ya pesa.maana au nia ya kukuambia hivyo ni ukiwa mfanyabiashara au mjasiria mali ifanye hela yako izunguke isiwe ya kukaa na kuhesabiwa tu.

5. Usiwe na tamaa

Ukiwa mfanyabiashara au mjasiriamali unatakiwa usiwe mtu wa tamaa, mtu ambae ukitamanishwa kitu mara moja umeshakitamani na unataka kuwa nacho hiyo ni mbaya kwa sababu ukiwa kwenye biashara utakutana na wafanyabiashara wengi na wa aina tofauti kuna wengine watakushawishi ujiunge na biashara zao, kuna wengine watakupa mawazo ya biashara nyingine inaweza kuwa ni kwa nia nzuri au mbaya lakini kitu kikubwa na cha msingi ni usiwe na tamaa simamia biashara yako hadi uhakikishe imefikia hatua uliyokuwa unaiota hapo ndio unaweza kuanza kufata ndoto za watu wengine .

6.Fanya biashara yako kwa mipango

Usifanye biashara kwa kupelekwa pelekwa panga mipango yako kabla ya kuanza kitu chochote na katika hiyo mipango usisahau kuweka plan b, ukiwa unapanga biashara yako kwa mipango itakupunguzia kuyumba kuyumba na pia kuyaona mafanikio au kushindwa kwa biashara mapema.

7. Brand biashara yako kwa hatua uliyopo.

Brand ina maana nyingi na ni kubwa lakini kwa ufupi ni Brand ni muonekano wa bidhaa yako na ahadi uliyoweka kwa mteja unayemtarajia ,lakini brand pia imegawanyika katika aina kuu nne ambazo ni alama , mfumo,mtu na bidhaa ambavyo vyote hivyo hufanya kazi pamoja ili upate mafanikio na majibu unayoyataka katika biashara ( nitaelezea siku nyingine kuhusu branding) hivyo kwa kuwa brand ndio msingi wa biashara na kuifanya brand kubwa ni gharama unatakiwa uifanyie brand yako kwa kila hatua unayokuwepo mfano: unaweza kuwa na kampuni ya kuuza kutengeneza unga lakini kwa kuanza hauna fedha ya kuibrand biashara unaweza kuanza kwa kufanya brand ya alama kwa maana ya muonekano wako kwa wateja wako, ukatengeneza nembo pamoja na vitu vichache vya kutumika ofisini baada ya hapo ukachapisha na mifuko ya kuwekea unga tayari hapo unafanya brand ya bidhaa yako ukimaliza hapo utakuwa unauza hadi ukiona unahama sehemu ya kwanza unaweza sasa kutengeneza mfumo kwa wafanyakazi wako kuwavalisha sare na baade pia kuanza sasa na kujitangaza hata kwenye mabango ya barabaani na kwenye runinga.

Tofauti ya matumizi ya pesa au vitu wanunuavyo watu wa Kipato cha Chini, watu wa Kipato cha Kati na Matajiri. huonekana ...
12/12/2015

Tofauti ya matumizi ya pesa au vitu wanunuavyo watu wa Kipato cha Chini, watu wa Kipato cha Kati na Matajiri. huonekana pale wanapo pata pesa
WEWE HUWA UNANUNUA NINI UNAPOPATA PESA AU MSHAHARA?

Adresse

MWANZA TANZANIA
Mwanza

Téléphone

+255768566054

Site Web

Notifications

Soyez le premier à savoir et laissez-nous vous envoyer un courriel lorsque 255 Young Rich Team publie des nouvelles et des promotions. Votre adresse e-mail ne sera pas utilisée à d'autres fins, et vous pouvez vous désabonner à tout moment.

Contacter La Pratique

Envoyer un message à 255 Young Rich Team:

Raccourcis

Partager