Ocean Road Cancer Institute

Ocean Road Cancer Institute Treatment,
Palliative care,
Research,
Diagnostic,
Prevention

Ratiba ya huduma ya tiba ya mionzi ya ndani
10/09/2026

Ratiba ya huduma ya tiba ya mionzi ya ndani

08/09/2026
08/09/2026

Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI) imeanza maandalizi ya kupata ithibati ya ubora wa huduma ikiwa tayari imefanya tathmini katika maeneo mbalimbali na kubaini mapungufu yanayohitaji kufanyiwa kazi ili kufikia viwango vya ubora vinavyotambulika kimataifa.

08/09/2026

Muonekano wa jengo la Kituo cha Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI) - Mbeya jinsi litakavyokuwa baada ya kukamilika kwa ujenzi

Taasisi ya Saratani Ocean Road imeanza maandalizi ya kupata ithibati ya ubora wa huduma ikiwa tayari imefanya tathmini k...
08/09/2026

Taasisi ya Saratani Ocean Road imeanza maandalizi ya kupata ithibati ya ubora wa huduma ikiwa tayari imefanya tathmini katika maeneo mbalimbali na kubaini mapungufu yanayohitaji kufanyiwa kazi ili kufikia viwango vya ubora vinavyotambulika kimataifa.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Kitengo cha Ukaguzi Tiba na Uhakiki Ubora wa ORCI, Hemed Myanza wakati akieleza hatua zilizofikiwa katika mchakato wa kupata ithibati, alipokuwa akizungumza na wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi katika kikao cha sita cha baraza hilo kilichofanyika hivi karibuni katika Hoteli ya Stella Maris wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani.

Myanza alisema katika maandalizi hayo ORCI imeweka mkazo katika kuhakikisha Taratibu za Kawaida za Uendeshaji (Standard Operating Procedures – SOPs) zinawekwa na kutumika katika maeneo yote ya taasisi ili kuwepo kwa mifumo na viwango vinavyofanana katika utoaji wa huduma.

Alisema hatua hiyo inalenga kuhakikisha kila eneo la huduma linafanya kazi kwa kuzingatia taratibu na viwango vilivyowekwa jambo litakalosaidia kuongeza ufanisi, usalama na ubora wa huduma zinazotolewa kwa wagonjwa.

Myanza alisema ORCI tayari imefanya mazungumzo na bodi zinazohusika na ithibati za kimataifa hatua inayolenga kusaidia taasisi kubaini chombo cha ithibati itakachoshirikiana nacho pamoja na kuelekezwa hatua zinazopaswa kuchukuliwa ili kufikia kiwango cha kupata ithibati ya kimataifa.

Kwa upande wao wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi waliupongeza uongozi wa ORCI kwa hatua mbalimbali za maboresho yanayolenga kuongeza ubora wa huduma na kuimarisha mazingira ya kazi huku wakisisitiza umuhimu wa kuunganisha uwekezaji katika miundombinu na vifaa vya kisasa na mifumo madhubuti ya utoaji wa huduma bora.

Naye Wamoja Mbonde ambaye ni Msimamizi wa Kumbukumbu za Afya alisema kupata ithibati kutakuwa hatua muhimu katika kuimarisha ubora wa huduma zinazotolewa na ORCI kwa kuwa kutaiwezesha taasisi kuwa na mifumo na viwango vinavyofanana katika maeneo mbalimbali ya utoaji huduma.

Kwa upande wake Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Saratani Faraja Kiwanga alisema mchakato wa kupata ithibati unapaswa kwenda sambamba na maboresho ya miundombinu, vifaa na mashine za kisasa yanayoendelea katika taaasisi hiyo.

SALAMU ZA POLEBodi ya Wadhamini, Menejimenti na Wafanyakazi wa Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI) tunatoa pole kwa Mh...
07/09/2026

SALAMU ZA POLE

Bodi ya Wadhamini, Menejimenti na Wafanyakazi wa Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI) tunatoa pole kwa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kufuatia kifo cha mume wake Mwalimu Hafidh Ameir Hassan, kilichotokea leo, Septemba 7, 2026 katika Hospitali ya Kumbukumbu ya Emilio Mzena, Zanzibar.

"Innalillah wainailaih rajuun"

“Saratani si hukumu ya kifo.” Huo ni ujumbe wa matumaini uliotolewa na Askofu Macha wakati wa uzinduzi wa Foundation yen...
07/09/2026

“Saratani si hukumu ya kifo.” Huo ni ujumbe wa matumaini uliotolewa na Askofu Macha wakati wa uzinduzi wa Foundation yenye lengo la kuhamasisha jamii kuondokana na hofu ya saratani na kuzingatia elimu sahihi kuhusu ugonjwa huo.

Akizungumza katika hafla hiyo Askofu Macha alisisitiza umuhimu wa jamii kupata taarifa sahihi kuhusu saratani huku akieleza kuwa hofu na dhana potofu zinaweza kuwafanya watu kuchelewa kutafuta huduma za afya.

Alisema kuwa saratani inapogundulika mapema mgonjwa anaweza kupata nafasi nzuri zaidi ya kupata matibabu na kuendelea na maisha yake. Hivyo, alitoa wito kwa wananchi kutopuuza dalili zinazoweza kuashiria ugonjwa huo.

“Tusisubiri mpaka ugonjwa uwe mkubwa", ni msisitizo unaobeba ujumbe muhimu kwa jamii: uchunguzi wa afya kwa wakati unaweza kuwa hatua ya kwanza ya kuokoa maisha.

Uzinduzi huo pia umeendelea kuimarisha wito wa ushirikiano kati ya taasisi za afya, viongozi wa dini, wadau na jamii katika kutoa elimu, kuhamasisha uchunguzi na kupunguza unyanyapaa kwa watu wanaoishi na saratani.

Naye Mwanzilishi wa taasisi hiyo Lydia Mcharo ambaye alipata matibabu ya saratani na kupona katika Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI) alisema kwa kuanzia taasisi hiyo itajikita katika mapambano dhidi ya saratani ya matiti na saratani ya mlango wa kizazi.

Lyidia alisema taasisi hiyo inalenga kuongeza uelewa wa jamii kuhusu umuhimu wa uchunguzi, kugundua saratani katika hatua za awali, kupata matibabu kwa wakati na kuwapatia wagonjwa msaada wanaohitaji katika safari ya matibabu.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI) Dkt. Diwani Msemo,Daktari bingwa wa Magonjwa ya Saratani Dkt. Kandali Samweli alisema kuanzishwa kwa True Rehoboth Cancer Foundation ni hatua inayoongeza nguvu katika jitihada za Serikali na wadau mbalimbali katika mapambano dhidi ya saratani nchini.

Dkt. Kandali alisema Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI) inapokea baadhi ya wagonjwa ambao wamefika katika hatua za juu za ugonjwa hali inayoweza kufanya matibabu kuwa na changamoto zaidi.

Address

Ocean Road, Luthuli Street
Dar Es Salaam
255

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Ocean Road Cancer Institute posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Ocean Road Cancer Institute:

Shortcuts

Share