Ocean Road Cancer Institute

Ocean Road Cancer Institute Treatment,
Palliative care,
Research,
Diagnostic,
Prevention

09/06/2026

ORCI kushiriki wiki ya utumishi wa umma yatakayofanyika mkoani Dodoma katika viwanja vya chinangali.....

Heri ya siku ya mashujaa Duniani...
07/06/2026

Heri ya siku ya mashujaa Duniani...

Je mwanamke umeshafanya uchunguzi wa Saratani ya Matiti na Mlango wa kizazi? K**a bado tunakukaribisha kufanya uchunguzi...
05/06/2026

Je mwanamke umeshafanya uchunguzi wa Saratani ya Matiti na Mlango wa kizazi? K**a bado tunakukaribisha kufanya uchunguzi huu hatua za awali, bila malipo yoyote...

02/06/2026
African Initiative Development Foundation (AIDF) ikiongozwa na Mkurugenzi wake Bw. Joel Temba kwa kushirikiana na Eden F...
31/05/2026

African Initiative Development Foundation (AIDF) ikiongozwa na Mkurugenzi wake Bw. Joel Temba kwa kushirikiana na Eden Foundation chini ya Mwenyekiti wake Bw Yesse Paschal kwa pamoja wamechangia damu katika Taasisi ya saratani ocean road.

Eden Foundation ni muunganiko wa wanafunzi kutoka vyuo mbalimbali.

Taasisi ya saratani ocean road imetoa shukrani na pongezi kwa wachangiaji waliochangia damu na kutoa wito kwa watu wengine kufika Taasisi ya saratani ocean road kwa ajili ya kuchangia damu.

Sherehe za wauguzi ORCI Katika picha.. ..........
30/05/2026

Sherehe za wauguzi ORCI Katika picha.. ..........

29/05/2026

Wauguzi kutoka Taasisi ya Saratani Ocean Road, (ORCI) mapema leo tarehe 29/05/2026 wamefanya maadhimisho ya siku ya wauguzi kwa kusherehekea pamoja na kula chakula na wagonjwa kutoka katika Taasisi hiyo.

Akizungumza katika sherehe hiyo, mkurugenzi wa huduma za wauguzi aliyestaafu Sr. Mary Haule amewataka wauguzi kuendelea kufanya kazi kwa kujitoa kwani ndio kazi ambayo wameichagua ili kusaidia wagonjwa.

Nae kaimu Mkurugenzi wa huduma za uuguzi ORCI Bi. Jenifer Mlingi amewasisitiza wauguzi kufanya kazi kwa moyo na kusimamia maadili ya kazi ili kuleta ufasaha wa kazi hiyo, kwani faraja kubwa ya wagonjwa ni kuwaona wao wakifanya kazi hiyo kwa ufasaha ili wapate afueni ya ugonjwa wao.

Aidha, mgeni rasmi ambae pia ndie kaimu mkurugenzi na pia ndie mkurugenzi wa huduma za kinga kutoka Taasisi ya Saratani Ocean Road Dkt. Crispin Kahesa amesema kuwa serikali ipo mbioni kuleta watumishi wapya na wengi wao ni wauguzi hivyo wasiwe na wasiwasi katika kushirikiana kwenye kazi.

Siku ya wauguzi Duniani huadhimishwa siku ya tarehe 12/05/2026 kila mwaka duniani kwa kumkumbuka mwanzilishi wake Bi. Florence Nightingale ambapo kwa ORCI sherehe yake imefanyika leo ili kutambua mchango wa wauguzi hao.

Eid al Adha Mubaraq...
27/05/2026

Eid al Adha Mubaraq...

Taasisi ya saratani ocean road katika kuboresha zaidi huduma kwa mteja katika taasisi, imeongeza zaidi kutoa mafunzo ya ...
27/05/2026

Taasisi ya saratani ocean road katika kuboresha zaidi huduma kwa mteja katika taasisi, imeongeza zaidi kutoa mafunzo ya huduma kwa mteja kwa watumishi wa Taasisi hiyo.

Mafunzo hayo yanafanyika katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere uliopo ndani ya majengo ya Taasisi ya saratani ocean road.

Mkuu wa kitengo cha Ukaguzi wa afya na Ubora wa huduma wa Taasisi ya saratani ocean road Dkt. Sadiq Siu wakati anatoa mafunzo hayo amewataka watumishi wote kuzingatia na kufanyia kazi yale yote wanayojifunza kwa vitendo Ili huduma ziwe bora zaidi.

Mafunzo hayo ya huduma kwa mteja ya siku tano, ambayo yanatarajiwa kumalizika tarehe 29/05/2026.

26/05/2026

Taasisi ya Saratani Ocean Road yamsindikiza King Sapeto mpaka nyumbani kwake baada ya matibabu ya Saratani...

Address

Ocean Road, Luthuli Street
Dar Es Salaam
255

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Ocean Road Cancer Institute posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Ocean Road Cancer Institute:

Share