13/06/2026
* Fangasi ukeni (vaginal yeast infection): Husababisha kuwashwa, muwasho, wekundu, maumivu wakati wa kukojoa au tendo la ndoa, na uchafu mweupe mzito. Usipotibiwa unaweza kuendelea kusababisha usumbufu mkubwa na maambukizi kujirudia.
* UTI (maambukizi ya njia ya mkojo): Husababisha maumivu au kuchoma wakati wa kukojoa, kukojoa mara kwa mara, mkojo wenye harufu kali au damu. Usipotibiwa, maambukizi yanaweza kusambaa hadi kwenye figo na kusababisha matatizo makubwa zaidi.
Ikiwa dalili ni kali, zinaendelea, au zinajirudia mara kwa mara, ni muhimu kumwona daktari kwa uchunguzi na matibabu sahihi.