31/07/2026
UGONJWA WA MKANDA WA JESHI (SHINGLES)
Huu ni ugonjwa wa ngozi na mishipa ya fahamu unaosababishwa na virusi aina ya ”varicella-zoster”, virusi hao ndio walewale wanaosababisha ugonjwa wa “tetekuwanga.”
Mara nyingi mtoto akiugua tetekuwanga akiwa kisha akatibiwa, virusi hivyo huwa havifi badala yake vinabaki kwenye mishipa ya fahamu kwa miaka mingi sana.
Sasa endapo itatokea kinga ya mwili ikashuka kwa sababu eidha umri mkubwa, kula vyakula visivyo na kinga kwa mwili, matumizi ya dawa za saratani, au dawa za kushusha kinga ya mwili — steroids, magonjwa ya saratani, virusi vya ukimwi na kisukari. Basi virusi hivi huamka upya na kuhambulia na kuleta mkanda wa jeshi.
�Dalili za mkanda wa jeshi.
Ugonjwa huu hushambulia upande mmoja wa mwili tu ndio maana uliitwa mkanda wa jeshi kwa kiswahili...inaweza kuwa Usoni-shingo au mgongo hadi tumboni. Kumbuka mkanda wa jeshi haupitilizi upande wa pili wa mwili. Bali uvimbe k**a wa mtu aliyeungua na majimaji hutokea sehemu zilizo athirika huku ukiambatana maumivu makali sana k**a ya moto na kuwasha.[moto wa mungu]
Dalili zingine ni k**a;
-Homa kali,
-Kichwa kuuma,
-Misuli kuuma,
-Uchovu mkubwa.
-Maumivu ya viungo
-Kuvimba kwa mitoki/matezi
�Mkanda wa jeshi kwa wajawazito.
Japokua sio kawaida kwa mama mjamzito kupata mkanda wa jeshi lakini anaweza kupata pia hasa akigusana na mgonjwa husika, hali hii ni hatari kwani husababisha kuathirika kwa mtoto aliyoko tumboni kwa kuzaliwa akiwa na matatizo ya kimaumbile.
�Jinsi ya kutambua ugonjwa huu
Daktari mzoefu anaweza kuutambua ugonjwa huu bila vipimo kabisa na kwa hospitali ambazo zina vipimo, huchukua majimaji ya upele ule na kupimwa ili kuhakikisha ni kweli ugonjwa ni wenyewe.
�Madhara ya mkanda wa jeshi
1. Maumivu makali baada ya kupona: Mgonjwa akitibiwa ugonjwa huu kwa baadhi ya dawa za hospitalini hata baada ya kupona maumivu makali ya sehemu zilizoathirika huendelea na mgonjwa huweza kurudi hospitali kwa kudhani bado ugonjwa haujaisha. Matibabu ya hali hii ni dawa