healthcareinfo_tz

healthcareinfo_tz Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from healthcareinfo_tz, Morogoro Referral Region Hospital, Morogoro.

05/09/2022

🎱 *vidonge vya kupanga uzazi*
🎱
👇🏿👇🏿👇🏿👇🏿
🥏Maamuzi ya aina ya uzazi wa mpango unaotaka kutumia ni jambo binafsi. Japo muhudumu hospitalini atakupa elimu juu ya faida na hasara za kila njia, kazi yako ni kuchagua ipi itakufaa. K**a unafanya tendo la ndoa mara kwa mara, kuna umuhimu wa kutumia vidonge vya uzazi wa mpango ili usishike mimba isiyotarajiwa.

🥏 *Jinsi vidonge vya uzazi wa mpango*
👇🏿👇🏿👇🏿👇🏿👇🏿👇🏿
🎱 vinavyofanya kazi
Vidonge vinafanya kazi kwa namna mbili. Moja vinazuia mayai kupevuka. Hii ina maana mifuko ya mayai haitatoa yai kwenye siku ya hatari, kwahivo hakutakuwa na yai la kurutubishwa na mbegu. Mbili Vidonge vinafanya uteute wa kwenye uke kuwa mzito sana. Ute mzito unazuia mbegu kuogelea na kwenda kurutubisha yai.

🥏 *Muda gani natakiwa kumeza vidonge* ????
👇🏿👇🏿👇🏿👇🏿👇🏿
🎱Ni muhimu kuendelea kumeza vidonge kila siku katika muda ule ule. Kupitisha hata masaa machache kunaweza kupelekea mayai yakapevuka na ukashika mimba (kikaumana)

🥏 *Ufanisi wa vidonge vya uzazi wa mpango ukoje?*

🎱K**a vikitumika ipasavyo, vidonge vinafanya kazi vizuri kuzuia mimba.
🎱ufanisi wa vidonge ni asilimia zaidi ya 91.

🧪Baadhi ya matibabu yanaweza kupunguza ufanisi wa dawa za uzazi wa mpango.

♟️Matibabu haya ni k**a👇🏿👇🏿👇🏿

🧩Baadhi ya antibiotics

🧩Dawa za Ukimwi k**a lopinavir na saquinavir

🧩Baadhi ya dawa za kifafa k**a carbamazepine na topiramate

🛝Dawa za uzazi wa mpango zinaweza kupunguza ufanisi pia kwa mgonjwa anayetapika na kuharisha.
🧪Endapo utakuwa na maumivu ya tumbo, zungumza na daktari akupime k**a uko kwenye hatari ya kushika mimba.
🧪 Unaweza pia kutumia njia nyingine k**a kondomu mpaka pale ukishapona.

🎱 *Zipi ni faida za kutumia vidonge vya uzazi wa mpango.*

Faida za vdonge ni pamoja na👇🏿👇🏿

🧩Kukukinga dhidi ya mimba isiyotarajiwa muda wowote unapofanya tendo

🧩Zinasaidia pia krekebisha mzunguko wa hedhi uliovurugika na hedhi nzito

🧩Siyo kizuizi cha moja kwa moja kushika mimba. Ukiamua kushika mimba unaacha tu kumeza vidonge.
🥳🥳🥳🥳🥳🥳🥳🥳

Upande wa Mbele wa Shingo kuna Tezi  muhimu inayoitwa Thyroid; tezi hii husisimua mwili kuchakata nishati.🔵Tezi hii inap...
15/06/2020

Upande wa Mbele wa Shingo kuna Tezi muhimu inayoitwa Thyroid; tezi hii husisimua mwili kuchakata nishati.

🔵Tezi hii inapokuwa tatizo la kushindwa kuzalisha homoni moja ya dalili ni mtu kushindwa kuhimili baridi lakini tatizo kuzalisha homoni kupitiliza mtu hawezi kuhimili joto

Shida kwenye ufanyaji kazi wa tezi ya thyroid huwa na athari kwenye ogani zote mwilini:
👉Moyo
👉Ngozi
👉Mfumo wa mmeng'enyo wa chakula
👉Afya ya akili
👉Mfumo wa uzazi
Uvimbe mbele ya shingo ni moja kiashiria cha tatizo kwenye tezi ya thyroid, unahitaji kuonwa na Daktari.

Cc:dr.normanJonas


Kuhusu Nishati-Mwili |
👉Iwapo tezi haizalishi homoni ya kutosha, mtuhuwa hawezi kuhimili baridi mfano maji ya baridi au chumba chenye AC au feni

👉Iwapo tezi hii inazalisha homoni kupitiliza;mazingira yenye joto yanakuwa shida Sana, mwili unachemka sana, unahitaji baridi zaidi

Leo ni siku ya kimataifa ya uchangiaji damu duniani.Kwa mujibu wa takwimu za Shirika la Afya Ulimwenguni za mwaka huu,wa...
14/06/2020

Leo ni siku ya kimataifa ya uchangiaji damu duniani.Kwa mujibu wa takwimu za Shirika la Afya Ulimwenguni za mwaka huu,wastani wa wanawake 800 wanaojifungua hufariki kila siku duniani kutokana na upungufu mkubwa wa damu. Kwa nchi za Afrika,zaidi ya 70% ya damu yote inayochangiwa hutumiwa na watoto wadogo wanaokabiliwa na upungufu mkubwa wa damu kutokana na ugonjwa hatari wa Malaria.
-
Pamoja na kukua kwa sayansi na teknolojia bado zoezi la utengenezaji wa damu bandia (mbadala) umegonga mwamba. Sehemu pekee tunayoweza kuipata damu ya binadamu ni kutoka kwa binadamu mwenzie. Ukiondoa kundi kubwa la akina mama na watoto,bado kuna makundi mengine ya watu wanaohitaji damu mfano watu wanaopata ajali kubwa. Ikiwa leo ni siku maalumu ya uchangiaji wa damu duniani,tujitoe kwa ajili ya maisha ya watu wengine. Changia damu,okoa uhai!

Mapafu ni ogani muhimu sana katika uhai, kila dakika unapumua wastani wa mara 15-20, hewa inayoenda na kukufanya uendele...
09/06/2020

Mapafu ni ogani muhimu sana katika uhai, kila dakika unapumua wastani wa mara 15-20, hewa inayoenda na kukufanya uendelee kuishi.

👉Mambo mbalimbali Huathiri mapafu.
DALILI ZINAZOWEZA KUASHIRIA UGONJWA MKUBWA KWENYE MAPAFU

1️⃣Kukuhoa Damu
- Muone Daktari hapohapo

2️⃣Shida ya kupumua, kifua kubana
-Hasa ukilala au ukifanya shughuri/zoezi ndogo kidogo unatafuta pumzi

3️⃣ Kikohozi zaidi ya wiki 2 hadi mwezi

4️⃣ Maumivu ya kifua
Hasa k**a yanauma zaidi unapokohoa au kupumua

5️⃣Pumzi kutoa mlio wa filimbi

MAFUTA MGANDO (Petroleum Jelly) yapo sokoni kwa zaidi ya karne moja na nusu; yameendelea kuaminiwa na madaktari bingwa w...
08/06/2020

MAFUTA MGANDO (Petroleum Jelly) yapo sokoni kwa zaidi ya karne moja na nusu; yameendelea kuaminiwa na madaktari bingwa wa ngozi k**a mafuta rafiki kwa ngozi hasa kwa watu wenye shida za ngozi k**a mzio, vidonda nk.

Mafuta ya mgando hutengeneza mazingira wezeshi ambayo huchochea vidonda hasa michubuko kupona haraka.Hupunguza uwezekano wa maambukizi kwenye vidonda vidogo kwenye ngozi.

Mafuta mgando husaidia afya ya ngozi na kupunguza dalili mbaya za magonjwa yatokanayo na mzio wa ngozi k**a pumu ya ngozi na magonjwa mengine k**a psoriasis.Hupunguza uwezekano wa kupata muwasho wa ngozi.

Mafuta mgando husaidia kupunguza mzio wa ngozi kwa watoto
Mzio wa ngozi husababisha ngozi za watoto kuwasha na kutoka mapele.Mgando huweza kutumika kwa mtoto kuanzia wiki 3. Mafuta mgando husaidia kuilinda ngozi ya mtoto dhidi ya vipele vya pampers (diaper rash) ambavyo husababishwa na mikojo/kinyesi kuathiri ngozi.Mafuta mgando hayana kemikali zaidi hivyo huwa rafiki kwa ngozi.

Mafuta mgando husaidia kupunguza maumivu kwa mtu mwenye bawasiri (hemorrhoid).Bawasiri huweza kusababisha maumvu wakati wa haja kubwa, mafuta ya mgando husaidia kupunguza hali hiyo.

Yalitengenezwa mara ya kwanza kusaidia vidonda kupona

Matumizi yaliongezeka hadi
-Kuzuia pua zisikauke hivyo kuzuia damu kutoka puani
-Kupunguza vipele sehemu za Siri visivyo magonjwa ya zinaa
-Kusaidia uponaji fangasi wa kucha nk

MUHIMU
Mafuta mgango hayafai kuwa kilainishi wakati wa kufanya mapenzi kwani huweza kuongeza uwezekano wa Kondomu kupasuka. Pia huongeza uwezekano kwa wanawake kuugua magonjwa ya uke hasa bacterial vaginosis

Credits:

Matatizo ya choo kigumu na bawasiri husumbua wanawake wengi wajawazito,wakati mwingine yakiendelea hadi wiki kadhaa baad...
07/06/2020

Matatizo ya choo kigumu na bawasiri husumbua wanawake wengi wajawazito,wakati mwingine yakiendelea hadi wiki kadhaa baada ya kujifungua. Sababu kubwa ya kutokea kwa tatizo hili ni uwepo wa mabadiliko makubwa ya vichocheo mwilini (homoni) pamoja na kutokea kwa mgandamizo mkubwa kwenye sehemu ya chini ya mirija ya damu (Lower abdomen veins) kutokana na kupanuka kwa mfuko wa uzazi pamoja na mtoto aliyehifadhiwa ndani yake.

Njia rahisi kabisa ya kutibu au hata kuepuka matatizo haya ni kujizoesha kunywa maji mengi,ulaji wa matunda na vyakula laini pamoja na kutumia mboga za majani kwa wingi. Mambo haya kwa pamoja yatasaidia kurahisha choo na kukuepusha dhidi ya changamoto hii. Kwa wanaojaribu njia hizi bila mafanikio wafike famasi au hospitali yoyote ya karibu kwa msaada zaidi.

Follow now;
Facebook & twitter

🔵Michirizi hutokea zaidi maeneo yenye mafuta k**a-TumboNI-Nyonga-Mapajani-Kalio-Matiti👉Michirizi haina shida kiafya wala...
07/06/2020

🔵Michirizi hutokea zaidi maeneo yenye mafuta k**a
-TumboNI
-Nyonga
-Mapajani
-Kalio
-Matiti

👉Michirizi haina shida kiafya wala madhara huweza kuisha yenyewe

👉Kuna njia mbalimbali za kitiba za kuiondoa kwa wale ambao hawaitaki ila matokeo hutofautiana mtu na mtu

🔵Michirizi hutokea zaidi maeneo yenye mafuta k**a
-TumboNI
-Nyonga
-Mapajani
-Kalio
-Matiti

👉Michirizi haina shida kiafya wala madhara huweza kuisha yenyewe

👉Kuna njia mbalimbali za kitiba za kuiondoa kwa wale ambao hawaitaki ila matokeo hutofautiana mtu na mtu

Follow now;
Facebook na Twitter

  | Unene uliokithiri (Obesity) unaongeza uwezekano wa kupata aina 13 za saratani:1️⃣Saratani ya matiti2️⃣Saratani ya ut...
06/06/2020

| Unene uliokithiri (Obesity) unaongeza uwezekano wa kupata aina 13 za saratani:

1️⃣Saratani ya matiti
2️⃣Saratani ya utumbo mpana na puru
3️⃣Saratani ya koo (adenocarcinoma)
4️⃣Saratani ya mfuko wa nyongo
5️⃣Saratani ya figo
6️⃣Saratani ya ini

Pata habari zaidi kwa kuendelea kupata kupakua sehemu mbalimbali za account zangu;
Facebook & Twitter

Iwapo unatarajia kubeba ujauzito Jitahidi kuanza kutumia virutubisho vya Foliki (Vitamin B9)👉Foliki uhitajika katika kuj...
31/05/2020

Iwapo unatarajia kubeba ujauzito Jitahidi kuanza kutumia virutubisho vya Foliki (Vitamin B9)

👉Foliki uhitajika katika kujenga ubongo wa mtoto tumboni

👉Ni muhimu katika miezi 3 ya kwanza ya ujauzito

👉Huzuia mtoto Kuzaliwa na ugonjwa wa kichwa kujaa maji na mgongo wazi.

Folic (Vitamin B9) ni kirutubisho muhimu ambacho huitajika ili mwili uweze kutengeneza DNA na RNA pia uweze kutumia virutubisho muhimu kwa ukuaji wa seli.

🔵Binadamu hawezi kutengeneza Folic lazima aipate kupitia lishe.

Zaidi ya 85% ya kesi za kujifungua mtoto mwenye ugonjwa wa mgongo-wazi au kichwa kujaa maji zinazuilika k**a mama akipata madini ya foliki kila siku miezi 6 kabla na kipindi chote wakati wa ujauzito.

Folic acid hupatikana pia katika vyakula k**a:
- mboga za majani zenye rangi ya kijani hususani spinachi
- Matunda jamii ya citrus (machungwa, chenza)
- Maharage, mkate, pia na nafaka zisikobolewa k**a Mchele wa kahawia

Cc:

UMUHIMU WA BAADHI YA VITAMIN MWILINICHANZO : Matunda & Mboga za majaniVITAMIN A 👉UMUHIMU : Afya ya macho, ngozi, ukuaji ...
31/05/2020

UMUHIMU WA BAADHI YA VITAMIN MWILINI

CHANZO : Matunda & Mboga za majani

VITAMIN A
👉UMUHIMU : Afya ya macho, ngozi, ukuaji wa mwili
👉UPUNGUFU : Ngozi dhoofu,Uoni hafifu, macho makavu , kutokuona usiku

VITAMIN D
UMUHIMU : Afya ya mifupa, kinga
UPUNGUFU : Mifupa dhaifu, matege

VITAMIN K
UMUHIMU : Uwezo wa damu kuganda
DALILI ZA UPUNGUFU : Uwezo mdogo wa kugandisha damu

VITAMIN C
UMUHIMU : Afya ya ngozi, fizi, uponaji wa vidonda, ufyonzaji chuma, kinga ya mwili
DALILI ZA UPUNGUFU: Fizi kutoka damu, maungio kuvimba, vidonda kutopoa, mafua mara kwa mara

VITAMIN B COMPLEXY (B1, 2,3,6 na 12)
UMUHIMU : Mwili kuzalisha nishati, afya ya Neva za fahamu, utengenezaji damu na kinga ya mwili
DALILI ZA UPUNGUFU : Kukosa hamu ya Kula, Hisia za uzuni, mdomo kupasuka, vidonda mdomoni, upungufu wa damu, akili kutotulia, ganzi

FOLIC ACID
UMUHIMU : Utengenezaji wa Seli za Mwili, Kuzuia mtoto Kuzaliwa na ulemavu hasa mgongo wazi na kichwa kujaa maji
DALILI ZA UPUNGUFU : Upungufu wa damu.

UMUHIMU WA KITUNGUU SWAUMU KATIKA NDOAKumekuwapo na tatizo la wanaume wengi kuwahi kufika kileleni, huku kitendo hicho k...
30/05/2020

UMUHIMU WA KITUNGUU SWAUMU KATIKA NDOA

Kumekuwapo na tatizo la wanaume wengi kuwahi kufika kileleni, huku kitendo hicho kikichanganywa na sababu mbalimbali ikiwamo mawazo na sababu nyinginezo.

Sifa kuu zinazokifanya kitunguu swaumu kuwa na uwezo na faida nyingi mwilini:

Vina uwezo wa kusababisha kutanuka kwa mishipa ya damu (vasodilation) kwa kubadilisha polysulfides zilizopo ndani yake kuwa hydrogen sulfides kwenye seli nyekundu za damu.

-Husaidia kuzibiti kiwango cha sukari mwilini kwa kushusha kiwango cha kemikali ya homocystine na hivyo

kupunguza madhara ya kisukari.

-Ukivikata vipande vidogo vidogo hivi (chop), vitunguu swaumu hutoa kemikali iitwayo kwa kitaalamu k**a ‘Allicin’ ambayo ni dawa dhidi ya bakteria, na ‘Phytoncide’ ambayo huua fangasi mbalimbali mwilini.

JINSI YA KUANDAA HICHO KITUNGUU:

1. Chukuwa kitunguu swaumu kimoja. Kigawanyishe katika punje punje

2. Chukua punje 6

3. Menya punje moja baada ya nyingine.

4. Kisha vikatekate (chop) vipande vidogo vidogo sana na kisu na uache hivyo katika hewa kwa dakika 10

Baada ya hapo meza k**a unavyomeza dawa na maji nusu lita kila unapoenda kulala. Namna nyingine nzuri zaidi ni kuviweka ndani ya kikombe kimoja (robo lita) cha mtindi freshi koroga vizuri na unywe na hii itakusaidia kupunguza harufu mbaya ya kitunguu swaumu.

Cc: Dr.Soy23

Facebook:
Twitter:

Katika kipindi hiki cha janga la COVID-19 kila mtu anafanya kila lililo ndani ya uwezo wake kujinusuru,na mojawapo ya ti...
26/05/2020

Katika kipindi hiki cha janga la COVID-19 kila mtu anafanya kila lililo ndani ya uwezo wake kujinusuru,na mojawapo ya tiba inayotumiwa na watu wengi ni Aloe vera. Tujifunze kidogo kuhusu mmea huu

Jamii zote za Aloe yaani Aloe barbadensis,A.africana,A.vera,A.spicata na A.ferox huwa na kiasi kikubwa sana cha madini ya sodium.Jamii ya watu wa Misri wanauchukulia mmea huu k**a mti wa uzima wa milele (plant of immortality),Wamarekani huuita the wand of heaven na Wahindi wakiupa jina la Kumari wakimaanisha binti/kijana mdogo mzuri,ambaye bado hajaona/hajaolewa

Sifa zote hizi zinatokana na utajiri mkubwa wa vitamin A,C,E,B1,B2,B3 (niacin),B6 na folate.Huwa pia na calcium,magnesium,zinc,chromium,selenium,chuma,potassium,copper,manganese na kiasi kikubwa sana cha madini ya sodium.Siyo hivyo tu,Aloe vera huwa na amino acids 20 kati ya amino acids 22 zinazotakiwa pamoja na amino acids 7 za muhimu kati ya amino acids 8 zinazotakiwa kwa afya ya binadamu

KWANINI SIYO SALAMA KWA WAGONJWA WA MOYO?
Pampu ya moyo hutumia mfumo wa pampu ya Na+/K+ ATPase.Pampu hii ya moyo hutoa nje unit 3 za sodium (3Na+) kwa kubadilishana na unit 2 za potassium (2K+) zinazoingia ndani ya seli za moyo.Kiasi kikubwa cha sodium kilichopo kwenye Aloe vera huusumbua uwiano huu hivyo kuidhoofisha pampu ya moyo katika kutengeneza mapigo yake.Watu wanaotumia dawa za kusaidia mioyo yao ifanye kazi vizuri wao pia hutumia mfumo huu huu katika kuboresha kazi ya moyo.

Kwa mantiki hii,Aloe vera husababisha kupungua sana kwa madini ya potassium kwenye damu hivyo kuidhoofisha pampu ya moyo,kubadilika kwa mapigo ya moyo,uchovu na kuongezeka kwa ukubwa wa tatizo la moyo.Pamoja na kuwa mgonjwa anaweza kuwa anatumia dawa (mfano digoxin) bado hatanufaika vizuri na tiba hii,maana uwezekano wa kuongezeka kwa tatizo ni mkubwa

USHAURI
Aloe vera hufahamika k**a mti wa maajabu kwa kutibu magonjwa mengi sana,pia katika kuongeza urembo wa ngozi na nywele.Kwa watu wasio na tatizo lolote lile la moyo wanaweza kutumia kwa kazi mbalimbali,lakini kwa wagonjwa wa moyo hawashauriwi kutumia mmea huu mara kwa mara hasa kwa kunywa kwani una hasara nyingi kwao kuliko faida zake!

Address

Morogoro Referral Region Hospital
Morogoro
11007

Telephone

+255657474814

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when healthcareinfo_tz posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to healthcareinfo_tz:

Shortcuts

Share