Dr. Buhanda na Afya Yako

Dr. Buhanda na Afya Yako “Follow Dr. Buhanda to learn simple health tips, how to prevent illnesses, and get health advice"

KISUKARI HAINA MAANA KWAMBA USILE MATUNDA...Tatizo siyo matunda, tatizo ni namna ya kula matunda, wakati wa kula matunda...
07/04/2026

KISUKARI HAINA MAANA KWAMBA USILE MATUNDA...

Tatizo siyo matunda, tatizo ni namna ya kula matunda, wakati wa kula matunda, kiwango cha kula matunda, aina ya matunda...

Follow Dr. Buhanda na Afya Yako.

UNAKULA UGALI K**A MLIMA KILIMANJARO USIKU, WALI, CHAPATI NANE, MIHOGO, VIAZI VITAMU, MAANDAZI, CHIPS HALAFU UNALALA MAR...
02/04/2026

UNAKULA UGALI K**A MLIMA KILIMANJARO USIKU, WALI, CHAPATI NANE, MIHOGO, VIAZI VITAMU, MAANDAZI, CHIPS HALAFU UNALALA MARA TU BAADA YA KULA, KIPI KINATOKEA MWILINI?

Fuatana nami. Naitwa Dr. Buhanda wa page yetu ya Dr. Buhanda na Afya Yako.

Fahamu kinachotokea ukilala muda mfupi baada ya kula baadhi ya vyakula k**a vilivyotangulia kutajwa.

✍ Kula ugali au wali usiku wala siyo tatizo, lakini kulala mara tu baada ya kula vyakula vyenye wanga mwingi hapo ndipo tatizo linaanza.

Nini hutokea?

Baada ya kula chakula chenye wanga mwingi (ugali, wali, mihogo, chapati, mikate nk)

** Sukari kwenye damu hupanda haraka.
Hii itachochea mwili kuzalisha insulin nyingi k**a kawaida yake ili isaidie kupunguza hiyo sukari nyingi mwilini. Hata hiyo kutokana na kwamba umelala sukari nyingi haitakuwa na matumizi mwilini na hivyo itabaki tu kwenye damu. Sukari inayobaki itahifadhiwa milini k**a mafuta, na hapa ndipo tatizo litakapoanzia k**a hiyo itakuwa tabia yako ya mwendelezo.

Matokeo yake ni;

⚠ Kuongehutoakwa uzito
⚠ Kuongezeka kwa mafuta tumboni
⚠ Hatari ya kupata Kisukari aina ya pili (Diabetes Melitus type 2)
⚠ Kusumbuliwa na kiungulia pamoja na gesi usiku
⚠ Kuamka tumbo likiwa limejaa gesi sana

SASA HAYO YOTE YANATOKEA KWA SABABU;
Kulala mara tu baada ya kula hupunguza sana mmeng'enyo wa chakula, mwili hautumii nishati ya kutosha. Nishati ni matokeo ya sukari kuunguzwa, kwahiyo sukari nyingi hubaki juu kwa mda mrefu.

Hii inaweza ikawa hatari zaidi kwa wenye uzito mkubwa sana, shida ya kisukari, na wenye tatizo la kusumbuliwa na gesi ( Gastroesophageo Reflux Disease-GERD)

SASA JE, KWA MAZINGIRA YETU TUNAWEZA KUEPUKA KULA UGARI?

Hata hivyo haina maana mtu asile ugali, wali, mihogo, chapati nk. Kumbuka hivyo pia huupa mwili nguvu, ni vyakula vinavyozalisha nishati kubwa mwilini. Kwahiyo ni vya muhimu.

Cha kufanya;

✅ Punguza kiasi cha ugali/wali na vingine k**a hivyo. Yaani k**a mpango ni kulala mapema basi angalau utumie kwa kiasi kidogo ili mwili ufanikiwe kudhibiti ongezeko la juu sana la sukari.

✅ Tembeatembea angalau dakika 10–30 baada ya kula. Hii huongeza uwezo wa umeng'enyaji wa chakula
✅ Kaa usubiri angalau saa 1–2 kabla ya kulala...Hii itakupunguzia kuvimbiwa tumbo, tumbo kujaa gesi na kuufanya mwili uwe active zaidi.

Mpangilio wa sahani yako mezani unaweza kuamua uamkeje, na afya yako kwa ujumla.

NB: Kwa elimu kuhusu afya yako, ungana na Dr. Buhanda na Afya Yako.

Like, share and comment...help growing others health

USISUBIRI MPAKA MIRIJA YA UZAZI IPASUKE, WAHI MAPEMA UOKOE AFYA YAKO YA UZAZI.Nadhani umewahi kusikia watu wakisema mimb...
26/03/2026

USISUBIRI MPAKA MIRIJA YA UZAZI IPASUKE, WAHI MAPEMA UOKOE AFYA YAKO YA UZAZI.

Nadhani umewahi kusikia watu wakisema mimba ilitungwa nje ya kizazi. HII IKIGUNDULIKA NI EMERGENCY, HAUTAKIWI KUKAA KWENYE FOLENI ILI UMUONE DAKTARI.

INATOKEAJE.
Kwa kawaida mimba inapaswa kukaa kwenye mfuko wa uzazi (uterus). Hapo ndipo inaweza kukua maana mfuko huo una uwezo wa kutanuka kadri mtoto anavyoongezeka.

Sasa huwa inatokea wakati mwingine baada ya yai la mama kurutubishwa kushindwa kushuka ili likakae kwenye mfuko wa uzazi. Hii inaweza ikatokea k**a mama amewahi kupata maambukizi kwenye mfumo wake wa uzazi, kitaalamu tunaita Pelvic Inflammatory Diseases (PID), au k**a mama amewahi kufanyiwa opereshen ya mirija ya uzazi, au k**a amewahi kuwa na Historia ya mimba nje ya kizazi nk. Sababu hizo zinaweza zikaathiri njia ya mirija hiyo na hivyo yai lililokwisha rutubishwa likakwama.

SASA IKIWA MIMBA IKO NJE YA KIZAZI, HIZI DALILI ZINAWEZA ZIKAJITOKEZA, UKIZIONA USIJISKILIZIE, CHUKUA HATUA MAPEMA.

✍1: Maumivu makali ya Tumbo.
Mama atahisi maumivu makali ya tumbo mwanzoni kabisa mwa ujauzito wake, hasa chini ya wiki 12 za ujauzito.
Hii ni kwa sababu mirija ya uzazi ni midogo sana kiasi kwamba haina uwezo wa kutanuka ili kusitiri mabadiliko ya yai linaloendela kubadilika kuwa kiumbe. Kwahiyo inabanwa hali inayopelekea maumivu makali sana na kutafsiriwa k**a maumivu ya tumbo, mara nyingi upande mmoja wa tumbo. Maumivu hayo yatasikika pia chini ya kitovu........
Ukiona dalili hiyo na katika wiki za mwanzoni kabisa, wahi kituo cha kutolea huduma za afya kwa uchunguzi zaidi.

✍2: Kutokwa Damu sehemu za siri.
Hii mimba hata ungeipa miaka mia haiwezi kukua. Hii ni kwa sabubu mwisho wa siku mirija ya uzazi itapasuka na matokeo yake ni damu kutoka sehemu za siri......
Ukiona hali k**a hiyo usikae nyumbani, wahi kituoni ukatibiwe.

✍3: Maumivu yanayoelekea mabegani.
Dalili zilizotangulia utazikuta kwenye changamoto mbali za uzazi. Lakini ukiona maumivu yanasambaa kuelekea mabegani na ukawa ulipima ikaonekana ni mjamzito, plus hizo dalili zingine, haraka sana nenda kituo cha kutolea huduma za afya ukapate uchunguzi zaidi maana hii ni dalili kubwa ya mimba nje ya kizazi.

✍4: KIZUNGUZUNGU AU KUPOTEZA FAHAMU.
Hii ni kwa sababu kupoteza damu kunapunguza ujazo wa damu (hypovolemia) hali ambayo hupelekea presha kushuka. Kushuka kwa presha kunapunguza mzunguko wa damu kwenda kwenye ubongo na hivyo ubongo 🧠 kukosa oxygen ya kutosha na hivyo mtu kupoteza fahamu........
Kwahiyo, ukiwa karibu na mama wa namna hiyo msaidie kufika kituo cha huduma za afya apate matibabu ya haraka kuliko kuhangaika kumpepea.

Dr. Buhanda na Afya Yako tunayo furaha kukujuza kwa uwazi kuhusu afya yako.
Follow page hii ya Dr. Buhanda na Afya Yako kwa updates nyingi zaidi.

us WhatsApp...0742 178 669

 ! “Unajua kuwa kupiga ultrasound katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito inaweza kuokoa maisha yako mama ...
24/03/2026

!
“Unajua kuwa kupiga ultrasound katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito inaweza kuokoa maisha yako mama na mtoto?”

Ngoja nikufundishe jambo ambalo litakusaidia kufikia hatima njema ya safari yako ya ujauzito.

Kipindi cha ujauzito huwa kitaalamu tunakigawa katika vipengele vitatu, kila kipengele kina miezi mitatu ambayo kwa ujumla hukamilisha miezi tisa ( Hii ndiyo miezi ya ujauzito kwa binadamu k**a hakuna changamoto nyingine)

Unachopaswa kufahaamu ni kwamba, kila kipengele huwa kuna kitu kinafanyika kwa mtoto awapo tumboni. SASA LEO NITAZUNGUMZIA KIPENGELE CHA KWANZA KABISA CHA UJAUZITO, YAANI MIEZI MITATU YA MWANZO YA UJAUZITTO ( First Trimester)

First Trimester ni kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo. Yaani ni sawa na wiki 12 za mwanzo za ujauzito.

Hiki ndicho kipindi ambacho kiumbe kinaanzwa kutengenezwa, naweza sema kuwa, huu ndiyo msingi wa ukuaji wa mtoto. Hapa viungo mbalimbali vya mwili winakuwa viko vinatengenezwa (organogenesis period). Ndiyo maana unahitaji kuwa makini sana na matumizi ya dawa katika kipindi hiki maana baadhi ya dawa zinaenda kuharibu moja kwa moja utengenezwaji wa viungo vya mwili na hiyo kusababisha kujifungua mtoto mwenye mapungufu fulani ( Congenital abnormalities)

Nadhani kwa sehemu umekielewa kipindi hiki cha miezi mitatu ya mwanzo.

SASA NAOMBA UNIRUHUSU KUENDELEA😂😂

Kufanya ULTRASOUND katika kipindi hiki ni muhimu sana kuliko kawaida. Kinaweza kikaamua hatima ya safari yako ya ujaaauzito.

HIZI NI FAIDA 6 MUHIMU SANA ZA KUFANYA ULTRASOUND KATIKA MIEZI MITATU YA MWANZO.

✍1. Itakusaidia kuthibitisha k**a ujauzito uko ndani ya mfuko wa uzazi na siyo nje.
✅Usiishie tu kushangilia kwamba umekuwa mama mtarajiwa, unapaswa kujiuliza kuwa; Je! Hii mimba imetungwa sehemu sahihi? Hii ni kwa sababu kuna kitu kitalamu tunaita (ECTOPIC PREGNANCY), hii ni mimba iliyotungwa nje ya mfuko wa kizazi. Inaweza ikawa kwenye mirija ya uzazi( fallopian tubes) au kwinginepo.

Hii mimba haiwezi kukua hata kidogo ikakupa mtoto. Na haiwezi kuvuka miezi mitatu (wiki 12), ikitokea ni mara chache sana na mwisho mirija ya uzazi itapasuka, mama atapata maumivu makali sana ya tumbo, atapoteza damu nyingi, atapoteza na fahamu na k**a asipopata huduma ya haraka atapoteza maisha hata yeye mwenyewe😔

Hayo yote yanaweza kuzuiliwa kwa kufanya kakitu kadogo ka gharama ndogo sana, yaani kupiga ultrasound.
ANZA KLINIKI MAPEMA, PIGA ULTRASOUND, OKOA MAISHA YAKO NA MTOTO.

✍2. Kujua umri sahihi wa ujauzito
Hii itakusaidia kupanga tarehe ya kujifungua kwa usahihi zaidi kuliko kukadiria kwa kutumia mfumo wako wa hedhi. USIBAHATISHE UMRI WA MIMBA, FANYA ULTRASOUND UWE NA UHAKIKA.

✍3. Kusikia mapigo ya moyo ya mtoto
Hii huwapa wazazi faraja kubwa ❤️. Inaongeza uhakika ya kwamba kuna usalama kwa mimba. K**a mapigo yakikosekana ujue kuna kasoro na daktari wako atakushauri cha kufanya.

✍4. Inakusaidia kugundua k**a ujauzito wako ni wa mapacha
Wengine hugundua mapacha mapema kabisa! Hii inakusaidia kutokuwa na wasiwasi hata ikitokea ukaona tumbo lako linaongezeka haraka kuliko kawaida.

✍ 5. Itakusaidia pia kugundua hatari za mimba kuharibika mapema.
Hii ni kwa sababu ultrasound itatujulisha k**a mimba ni ya mapacha, either wawili, watatu au zaidi. Hizi mimba huwa zinahitaji uangalizi mkubwa sana maana zina hatari ya kuharibika. Lakini pia ultrasound itakusaida kujua k**a mimba iko sehemu sahihi, mimba isiyo sehemu sahihi haiwezi kukua. Utajua pia k**a kuna mapigo ya moyo. Ultrasound inaweza kugundua mapigo ya moyo mapema kabisa kuanzia wiki ya 6. Yakikosekana basi ufuatiliaji utahitajika sana.

✍6. Ultrasound itakusaidia kujua k**a hiyo ni mimba halisi.
SIYO KILA MIMBA NI MIMBA...UTANIELEWA SOMO LIJALO, USIACHE KUFUATILIA.

MASWALI NINAYO KUTANA NAYO KWA WAMAMA WENGI NI PAMOJA NA HILI;

Je, ultrasound ina madhara kwa mtoto?
Jibu ni fupi tu:
👉 Hapana. Ultrasound haina madhara kabisa kwa mtoto, yenyewe hutumia mawimbi ya sauti, siyo mionzi k**a X-ray.

Kwa masomo mengi kuhusu afya yako;
Follow Dr. Buhanda na Afya Yako


Wasiliana na Dr. Buhanda WhatsApp 0742 178 669 kwa ushauri zaidi.

24/03/2026

HUITAKI PRESHA?
Fanya haya mambo matano kwa uaminifu na kwa mwendelezo...
Dr. Buhanda na Afya Yako

DOKTA, HIVI KUNA KINGA YA PRESHA?😂😂Ni swali nililowahi kuulizwa na mama mmoja aliyekuwa na hofu kubwa ya  kuugua presha ...
23/03/2026

DOKTA, HIVI KUNA KINGA YA PRESHA?😂😂

Ni swali nililowahi kuulizwa na mama mmoja aliyekuwa na hofu kubwa ya kuugua presha maana alikuwa ameondokewa na mpendwa wake kwa shida hii ya Presha.

Nilimjibu kwa urahisi, ndiyo, kuna namna tunaweza kujikinga na presha k**a hatutaki kuhakangika na kuja kutibu presha. HAKUNA CHANJO YA PRESHA, HILO ULIJUE!

Wengi waliokutwa na presha haikuanza tu ghafla, sometimes unaweza usione dalili ila ikawa ipo ingawa matokeo yanaweza yakaonekana ghalfa.

Yaani ni ghafla tu mtu anasikia mapigo ya moyo k**a hayaelewi. Ni ghafla anaona mwendelezo wa maumivu ya kichwa, ni ghafla mtu anaweza pata kiharuse (stroke). Hiyo hgafla unaweza ukawa ndo umeiona wewe ili msababishaji (presha) alikuwepo kitambo.

SASA KUEPUKANA NA HAYO YOTE, TUJITAHIDI KUFANYA HAYA, KWA SEHEMU KUBWA YATATUSAIDIA. Yapo mengi ya kufany, ila anza na haya ambayo hayana gharama. Najua umewahi kuyasikia, usiyadharau😂😂 leo utayaelewa vizuri yanavyosababisha presha.

✔ Punguza chumvi kwenye chakula chako.
Kuna wale tuliwahi kusema wekeni chumvi nyingi ili tunywe maji mengi hasa k**a chakula ni kidogo kutosha familia nzima 🤔. HIYO HAIKO KITAALAMU KABISA.

Kwanini uipunguze chumvi. Kwenye chumvi kuna madini ya Sodium, haya yana kazi nyingi mwilini ikiwa ni pamoja na kusafirisha taarifa mwilini katika mfumo wa umeme (nerve impulse transmission).

Sasa mbali na kazi hiyo nzuri, Sodium pia inayopatikana kwenye chumvi huwa inasababisha mwili ushikilie maji (water retention). Huwa Sodium ions zinasambaa kwenye damu. Zikiwa kwenye damu, damu inakuwa highly concentrated ( blood become more hypertonic than extracellular fluid). Kitendo ambacho kitasababisha maji yatoke kwenye seli zingine za mwili ili kwenda kupoza hicho kiwango kilichozidi kwenye damu na kuziacha cell za mwili zimenyauka(shrikns)

Sasa kuongezeka kwa maji kwenye damu maana yake ni volume(ujazo wa damu) inaongezeka, kwa hiyo damu inasukuma kuta za mishipa ya damu kwa nguvu hali ambayo hupelekea kuongezeka kwa presha.

KWAHIYO UNAWEZA KUONA, CHUMVI INAMCHANGO MKUUBWA KWENYE KUPANDISHA PRESHA. Kwa mwenye presha apunguze chumvi, kwa ambaye hana azuie chumvi nyingi.

✔ Fanya mazoezi
Aise, ni kakitu kadogo ila katatusaidia. Mazoezi yana namna nyingi yanavyoweza kupunguza au kuzuia shinikizo la damu.
**Mazoezi yanasaidia kuunguzwa kwa mafuta mwilini, hii hupelekea kulinda mishipa ya damu kwani mkusanyiko wa mafuta kwenye mishipa ya damu hautakuwepo. Kwa hiyo njia ya mishipa ya damu haitapungu (no atherosclerosis-arterial wall thickness). Matokeo yake Damu itasafiri bila kupata uzuizi/ upinzani na hivyo presha haitakuwepo. Hapo utakuwa umeulinda na moyo wako (Moyo hautatumia nguvu kubwa kusukuma damu)

**Pili Mazoezi yatasaidia kuifanya mishipa ya damu kupanuka vizuri. Mazoezi huifanya mishipa iwe yenye elasticity, kitendo kinachoifanya ipanuke vizuri. Mishipa inayovutika/kupanuka vzr hupunguza upinzani wa damu na hivyo nguvu kidogo kutumika kusukuma damu ikiwa na maana presha haipandi.
anakushauri ufanye mazoezi, mazoezi ni afya. Tumia angalau nusu saa kila siku asubuhi au jinoni, ukiweza asubuhi na jioni kutembea, kukimbia taratibu, kuruka kamba nk. Hapo presha yako utaidhibiti.

✔ Penda kula kiasili.
Kwa bahati mbaya sana utandawazi na umjini umetuathiri. ✍✍Mifumo mbalimbali ya mwili inakufa kwa kujazwa vyakula vyenye kemikali nyingi na madawa. Ni kweli ni vitamu😂 ila vyaku vyenye mafuta mengi k**a chips, vyakula vya kusindikwa, vinywaji vyenye sukari artificial ni adui wa mifumo mbalimbali ya mwili.

Tengeneza juisi yako mwenyewe kwa kutumia matunda asili na viungo asili k**a maparachichi, malimao, tangawizi, hoho, nk. Hivyo vitasaidia sana kuimalisha afya ya mfumo wa mzunguko wa damu na kukuepusha na presha. Si hivyo tu, vitakupa pia hata kinga dhidi ya magonjwa.
Tembea na silogani hii...MBOGA ZA MAJANI NI NYAMA INAYOOTESHWA, CHIPS INAYOOTESHWA, JUISI INAYOOTESHWA😁😁 ...hiyo itakusukuma kutumia mbogamboga asili badala ya vyakula hatarishi kwa afya yako.

✔ Jitahidi kudhibiti msongo wa mawazo.
Msongo wa mawazo ni msaidizi mkubwa sanaa wa presha kuinuka.
Mwili wa binadamu una hormone ya adrenaline na Cortisol. Hizi zikiongezeka zinapandisha presha. Sasa mazingira yanayoweza kuzipandisha hizo homoni ni pamoja na msongo wa mawazo. Msongo wa mazo ukiwepo huwa na zenyewe zinazalishwa sana, zikizalishwa sana mapigo ya moyo yanaongezeka (ndo pale mtu anakwambia nasikia moyo unakimbia😔). Nisiende mbali sana kueleza inavyokuwa nisikupoteze, ila mwisho wa yote mwendelezo wa hali hii ni presha kutokea.

EASY TO REMEMBER: Avoid stress, avoid hyper-secretion of stress hormones, avoid rapid heart rate, Avoid arterial flow resistance, avoid pressure

✔ Tumia dawa ipasavyo
Hii ni kwa wale ambao tayari walisha pima presha yao mara kadha na wahudumu wa afya na kufikia hitimisho la kuambiwa wana shida ya presha. Nimekutana na case nyingi, wengi wanakuja kujieleza kwa kutoa maelezo yanayotaka dakitari ajifunge kwa kuwaambia waache kutumia dawa. JIBU LANGU HUWA NI MOJA TU, TUMIA DAWA, UKIACHA UTAKUFA GHAFLA.

Nakushauri leo, usiache dawa mpaka daktari wako akupe maelekezo mengine. Dawa sahihi, matumizi sahihi, wakati sahihi zina nafasi kubwa sana ya kukufanya ubaki salama dhidi ya madhara yatokanayo na preshaa k**a Figo kuathirika, ubongo, moyo na kukuepusha na kiharusi (Stroke)

✔ Jenga mazoea ya kupima Presha yako.
Huu nao ni ustaarabu mzuri sana. Usipime presha baada ya kush*tuliwa na presha. Jiwekee utaratibu wa kupima presha mara kwa mara, angalu mara moja kwa mwezi (Kupima mara nyingi zaidi kuna salama)

NB. Hakikisha unapima kwenye kituo cha kutolea huduma za afya chenye wataalamu wanaoelewa kuhusu presha.
..Kwa sehemu anza hivyo, presha itakuwa mabali na wewe...
Dr. Buhanda na afya yako

HONGERA NA KARIBU SANA.Je, unajua afya ni kitu pekee ambacho kikipata hitilafu hakihitaji useme huna hela?  Dr.Buhanda n...
21/03/2026

HONGERA NA KARIBU SANA.

Je, unajua afya ni kitu pekee ambacho kikipata hitilafu hakihitaji useme huna hela?

Dr.Buhanda na Afya Yako ni page yetu mpya ambayo imeundwa rasimi kwa ajili ya kukusaidia wewe kupata ushauri wa bure kuhusu afya yako. Utapata utatuzi wa changamoto mbalimbali za kiafya ambazo umekuwa ukikutana nazo au kusikia kwa watu wako wa karibu.

Dr. Buhanda page itakupa ruhusa ya kushare changamoto yako ya kiafya inayokusumbua kipekee (privately) kwa njia ya kupiga simu, kuchati au kupitia WhatsApp.

Lakini pia ikiwa utakuwa na uhitaji wa kutaka kujua chochote kuhusu afya utapata nafasi ya kushare nami concern yako nami nitakuandalia kipindi ambacho nitakiwasilisha kwenye page yetu ili na wengine wajifunze.

NJIA ZA KUJIFUNZA KATIKA PAGE YETU HII.

1: Tutakuwa tunatumia video fupifupi zitakazokuwa zinarushwa ndani ya page hii kutoka kwa Dr. Buhanda.

2: Tutakuwa tunatumia slides zitakazokuwa zinaandaliwa na Dr. Buhanda

3: Tutakuwa tunatumia njia ya uandishi ambapo utakutana na jumbe mbalimbali kuhusu afya kutoka kwa Dr. Buhanda.

KIPI KIZURI KUHUSU PAGE HII.

Nafarijika kwamba siku hizi wataalamu wengi wamejikita kufundisha jamii mambo mbalimbali kuhusu afya kupitia mitandao, I appreciate!

Sasa Dr. Buhanda page ni page itakayoungana na wataalamu wengine kuhakikisha inaifikia jamii na kufundisha kuhusu afya.

TOFAUTI na wataalamu wengine, Dr. Buhanda page ni page pekee itakayowasilisha maudhui yake kwa njia rahisi sana itakayoeleweka na yeyote bila kujali amesoma au la! Nimelenga kutumia lugha ya kawaida sana na ya rahisi kueleweka ili kila mtu afaidike na page hii.

: Badala ya kusema (SABABU ZA ) kitu ambacho wengi hawataelewa, badala yake nitakuambia (SABABU ZA MOYO KUTANUKA/ KUWA MKUBWA KULIKO KAWAIDA) Hapo ndipo nitakuelezea kwa urahisi na hatua za kuchukua.

Lakini pia nitajikita kukuletea mafunzo ya vitu ambavyo tunakutana navyo kwa urahisi.

Kwa mfano; badala ya kukufundisha namna DVT (Deep Venous Thrombosis) inavyotokea, topic ambayo inapaswa kuwasilishwa kwa watu wa namna fulani, au ikiwa ni kwa wote basi kutumia mifano mingi sana ili kuelewa, badala yake nitakufundisha vitu k**a, ULAJI RAFIKI KWA MWENYE SHIDA YA SUKARI. Hicho ni kitu ambacho yeyote anaweza akawa interested na akaelewa.

CHA KUFANYA SASA
Follow page yetu ili kila tutakapoweka mada mpya basi upate taarifa na ufuatilie na kujifunza. Share page yetu pia na kwa watanzania wengine ili nao wasipitwe...

Utakuwa nami Dr. Buhanda (Mganga Mfawidhi El-Shaddai Dispensary-Tabora Tanzania)

Address

Tabora

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Dr. Buhanda na Afya Yako posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share