02/08/2026
MPIGA GITA WA ZAMANI WA FALLY IPUPA (ALVARITO SOLO) AMEFARIKI DUNIA
LE DÉCÈS DE ALVARITO SOLO, ANCIEN SOLISTE DE FALLY IPUPA.
Nkondi Alvarito, anayefahamika k**a Alvarito Solo, ni miongoni mwa wapiga gitaa wachache wa Congo ambao ustadi wao hauishii kwenye ujuzi tu, bali unafikia kiwango cha fasihi ya sauti.
Alizaliwa Jijini Kinshasa, katika mazingira ya Muziki yaliyokuwa yakichemka kila kona la jiji.
Katika miaka ya tisini, aling’aa wakati akichangia na Group (Stars Musica) Jijini Kinshasa Lingwala, akionyesha kipaji cha kipekee kilichowavutia wakongwe wa rumba.
Baadaye alijiunga na Wenge El Paris ikiongozwa na Marie‑Paul, kadhalika na Wenge Kumbela ya Aimé Bwanga, ambako alithibitisha kuwa MPIGA Solo Gita wa kiwango cha juu.
Safari yake ilipata hadhi ya juu zaidi alipoingia katika F’Victeam, Group lake Fally Ipupa.
Hapa alitunga wimbo wake maarufu (Rosendane), na akashiriki katika nyimbo kadhaa za Album (Libre Parcours) k**a Toi et Moi, Original, na nyimbo za nyingi zilizojaa ustadi wake wa kipekee.
Gitaa lake lilikuwa na mchanganyiko wa huzuni, uzuri na hisia za ndani ambazo ziligusa mioyo ya wasikilizaji.
Mbali na hapo, Alvarito alishirikiana na Héritier Watanabe, Pierrette Adams, na Wasanii wengine wa Congo na nje ya nchi.
Aliunda pia Group lake mwenyewe wakati akiwa Nchini Angola, akionyesha dhamira ya kueneza rumba ya Congo kimataifa.
Lakini nyuma ya mafanikio haya, Alvarito alikuwa akipambana na shinikizo la damu kwa muda mrefu.
Tiba za hospitali hazikumletea nafuu. Katika kipindi hiki cha majaribu, aliamua kutafuta uponyaji wa kiroho kupitia makanisa ya Walokole.
Hatua hii haikuwa ya ghafla; ilikuwa matokeo ya safari ya ndani ya kutafuta amani.
Hatimaye akawa mwimbaji wa injili, akigeuza gitaa lake kuwa chombo cha kumtukuza Mungu.
Tarehe 1 Agosti 2026, Alvarito alifariki dunia huko Kinshasa, na Muziki wa Congo ukaingia katika huzuni kubwa.
Wasanii, Marafiki na Mashabiki walimkumbuka k**a Mtu mnyenyekevu, mwenye moyo wa upendo na kipaji kisicho na kifani.
Leo, urithi wake unaendelea kuishi katika sauti za gitaa zinazopigwa mitaani ya Jiji la Kinshasa.
Kila mpigo wa nyuzi unabeba kumbukumbu yake.
Alvarito Solo anabaki kuwa mfano wa Msanii wa Congo anayefanya gitaa liimbe k**a sauti ya binadamu, na sasa sauti hiyo inaendelea kumtukuza Mungu.
Version Française :
Nkondi Alvarito, connu sous le nom d’Alvarito Solo, appartient à cette lignée rare de guitaristes congolais dont la virtuosité ne relève pas seulement de la technique, mais d’une véritable poétique sonore.
Né à Kinshasa, il grandit dans l’effervescence musicale de la capitale, où les guitares de Lingwala, Bandalungwa et Matonge façonnaient les destins artistiques.
Dans les années 1990, il se distingue au sein du groupe Stars Musica, formation emblématique de la commune de Lingwala.
Son jeu, déjà empreint d’une sensibilité singulière, attire l’attention de figures majeures de la rumba.
Il rejoint alors Wenge El Paris de Marie‑Paul, où il affine son style, puis Wenge Kumbela d’Aimé Bwanga, formation dans laquelle il confirme son statut de soliste d’exception.
Sa carrière prend une dimension supérieure lorsqu’il intègre F’Victeam, le groupe de Fally Ipupa.
Là, il compose le célèbre titre (Rosendane), devenu une pièce incontournable du répertoire moderne.
Il participe également à plusieurs morceaux de l’album Libre Parcours, notamment Toi et Moi, Original, et divers génériques où sa guitare, à la fois mélancolique et lumineuse, impose une signature immédiatement reconnaissable.
Outre ces collaborations, Alvarito travaille avec Héritier Watanabe, Pierrette Adams, et accompagne divers artistes de la scène kinoise et internationale.
Il fonde même un groupe en Angola, témoignant de son ambition de porter la rumba au-delà des frontières.
Cependant, derrière cette ascension artistique se cache une lutte silencieuse : Alvarito souffrait depuis longtemps d’une hypertension sévère, affection qui minait progressivement ses forces.
Malgré les traitements médicaux, son état ne s’améliorait pas.
Dans cette période de fragilité, il se tourne vers les églises de réveil, cherchant une guérison spirituelle.
Sa démarche n’est pas opportuniste : elle traduit une quête intérieure profonde.
Il finit par se convertir, devenant chantre de l’Éternel, transformant sa guitare en instrument de louange.
Le 1er août 2026, il s’éteint à Kinshasa, laissant la communauté musicale dans une stupeur douloureuse.
Les hommages affluent : réalisateurs, musiciens, anciens collègues évoquent un homme humble, généreux, d’une loyauté rare et d’un talent hors du commun.
Son décès marque la disparition d’un soliste dont la guitare semblait parfois parler à la place du cœur humain.
Aujourd’hui, son héritage résonne encore dans les rues de Lingwala, Bandal, Matonge.
Chaque arpège qui s’élève dans une répétition, un studio ou un concert porte quelque chose de lui.
Alvarito Solo demeure l’incarnation de cette rumba qui sait pleurer, sourire, prier et célébrer une rumba qui, grâce à lui, continue aussi de glorifier Dieu.
BABA L.W.L