21/05/2026
P.I.D ni kifupi cha Pelvic Inflammatory Disease, yaani Ugonjwa wa Maambukizi ya Sehemu ya Juu ya Mfumo wa Uzazi kwa Mwanamke.
Maana yake Ugonjwa huu ni Hii:
Ni maambukizi ya bakteria yanayoathiri maeneo k**a:
- Kizazi (uterus)
- Mirija ya ya uzazi ambayo hufanya kazi ya kupitisha yai (fallopian tubes)
- Ovari
- Kuta za kizazi (Uterine lining (endometrium)
P.I.D Husababishwa na nini?
- Maambukizi ya magonjwa ya zinaa hasa Chlamydia na Gonorrhea
- Kutumia vifaa visivyo safi vya uzazi (mfano IUCD)
- Kutoka mimba au upasuaji usio salama
- Kuosha uke kwa ndani mara kwa mara Kwa kuingiza vidole (douching)
Dalili kuu Za P.I.D:
- Maumivu chini ya tumbo
- Uchafu mwingi ukeni wenye harufu mbaya au usio na Harufu.
- Maumivu wakati wa tendo la ndoa
- Homa na uchovu
- Maumivu ya mgongo au kiuno
- Kutokwa damu katikati ya mzunguko
Madhara yake:
- Ugumba (kutopata mimba)
- Mimba ya Kutunga nje ya kizazi
- Maumivu sugu ya nyonga
- Mimba kuharibika mara Kwa mara
MUHIMU: Tiba mapema inaepusha madhara makubwa.