10/10/2022
Utafiti uliofanywa na Shirika la Afya Duniani (WHO) umeonyesha kuwa, takriban mtu mmoja kati ya kila watu nane duniani ana changamoto ya ugonjwa wa akili. Taarifa hiyo inaendelea kuonyesha kuwa kila kifo kimoja kati ya vifo 100 duniani husababishwa na mtu kusitisha uhai wake mwenyewe. Asilimia 50 ya vifo hivyo hutokea kwa watu wenye umri chini ya miaka 50. Kujiua imeelezwa kuwa ni sababu moja wapo kati ya sababu kuu zinazo pelekea vifo vya watu katika umri wa miaka 15-29. Kwa nchi yetu ya Tanzania, inakadiriwa kuwa na watu takribani millioni saba wanapitia changamoto za afya ya akili, wanawake wakitajwa kua ni kundi linalo athiriwa zaidi na changamoto hizi.
Afya ya akili imetajwa kuwa muhimu si tu katika ubora wa maisha lakini pia katika maswala ya uchumi na uzalishaji.
Jali Afya kwa ajili ya maisha Bora