24/02/2023
Part 2
Baada ya kujifungua…..
Hapa wengi mnakua mnafikiri hawa wakina mama wanakua na furaha k**a ambavyo mnawafurahia na kuwapa hongera nyingi,
Kwanza mpunguze kwenda kuwaona,wanahitaji sana muda wa kuwa na mtoto na familia yake pamoja na kupumzika,
Mambo huwa tofauti.Wengine wanapata postpartum depression,wanaendelea kutuhitaji sana wataalam wa afya na pia katika kipindi hiki wanahitaji wasaidizi au ndugu ambaye anahitaji pia kufundishwa namna ya kuishi naye,asimchanganye kabisa na mambo yake,asimchanganye na kumfundisha kila aina ya malezi…
1. Bado wanajiuliza hivi ni mimi kweli nimepata mtoto?
2. hawawezi kulala hata k**a kuna mtu wa kumsaidia kukaa na mtoto
3. Wanashindwa kula vizuri
4. Wanahisi kila anachokifanya inawezekana atakosea mtoto atapata tatizo
Unaweza usigundue haya kwa ndugu yako unayeishi naye ambaye alihangaika kutafuta mtoto kwa muda mrefu,
Ila japo Hakikisha anatembelewa na mtoa huduma kumfanyia uchunguzi wa namna anavyoishi,
Sio kwamba anamlea mtoto k**a yai,sio kwamba anakua mkali,ana panic ndo hali halisi mnatakiwa mumuelewe,vaa kiatu chake,
Wanatakiwa kuhudumiwa kwa uangalifu sana sana na kuelekezwa kwa kitaalam sana na wakati mwingine mzindue akili arudi kwenye dunia ya kawaida😀,Wana mambo yao special na si ya kupuuza…