Dr. Christopher Cyrilo

Dr. Christopher Cyrilo Medical Doctor| Health Literacy expert | Social Activist | Writer

Uzazi wa Mpango! Ni njia gani unayopendelea kutumia kupanga uzazi?   Wanawake wengi wanatoa malalamiko yanayotokana na m...
30/04/2026

Uzazi wa Mpango!
Ni njia gani unayopendelea kutumia kupanga uzazi?

Wanawake wengi wanatoa malalamiko yanayotokana na matumizi ya dawa za uzazi wa mpango. Malalamiko ni mengi. Ingawa wataalamu tunasema kuna maudhi madogo madogo yatokanayo na matumizi ya dawa za uzazi wa mpango, lakini kwa idadi fulani ya wanawake inaonekana maudhi hayo si madogo.

Je! Umewahi kutumia njia yoyote ya uzazi wa mpango?
Una uzoefu gani juu ya maudhi yanayotokana na matumizi ya dawa za uzazi wa mpango?
Umeongezekwpa uzito kupita kiasi (umenenepeana)?
Uke unakuwa mkavu sana?
Unapata mzunguko wa hedhi bila mpangilio? Maumivu huwa makali na damu huwa nyingi au kidogo kuliko kawaida?
Kichwa kuuma mara kwa mara?
Unajisikia kuchokachoka?
Umeacha kutumia uzazi wa mpango (sindano vidonge) na sasa unataka ujauzito lakini hupati?
Unadhani changamoto hizi kubwa zinatokana na ubora mdogo wa dawa zinazotumika? Au hata katika nchi zilizoendelea changamoto hizi zipo?
Ni uzoefu wako binafsi, au umesikia, umeshuhudia?

Unadhani ni zipi njia sahihi za uzazi wa mpango ambazo mtu anaweza kutumia bila maudhi au kwa maudhi yanayovumilika?

Niambie!
Dr. Chris Cyrilo.
Nawasilisha!


Munyonyo - Kampala, Uganda. Katika mkutano wa 5 wa Kansa na Tiba Shufaa (Palliative Care). Shule kidogo! Kansa sio ugonj...
28/02/2026

Munyonyo - Kampala, Uganda.
Katika mkutano wa 5 wa Kansa na Tiba Shufaa (Palliative Care).

Shule kidogo!
Kansa sio ugonjwa mmoja, ni kundi la maradhi mengi yanayoweza kufikia hata 100 au zaidi.

Karibu kila kiungo mwilini kinaweza kuathiriwa na kansa. Moyo pekee ndio ogani ambayo ni vigumu sana kupata kansa inayochipukia kwenyw moyo wenyewe, isipokuwa unaweza kuathiriwa na kansa kutoka kwenye ogani nyingine.

Kuna kansa ya Ubongo, kansa ya koo, kansa ya tumbo, kansa za utumbo mdogo, utumbo mkubwa, kansa ya kibofu, kansa ya uume, kansa kinywa, kansa ya jicho, kansa ya ulimi, kansa ya koromeo, kansa ya umio, kansa ya tezi mbalimbali (thyroid, adrenal nk), kansa za ngozi, kansa za mifupa, kansa za damu, kansa ya kongosho, kansa ya figo, kansa ya ini, kansa ya matiti, kansa ya shingo ya kizazi. Kansa ni nyingi sana. Binadamu ana ogani zinazokadiriwa kuwa 78 na karibu zote zinaweza kupata kansa.

Bado haitoshi, kuna aina za kansa kwa kutegemea aina ya seli au tissue zilizoathiriwa. Mfano, ngozi ya mwanadamu inaundwa na aina nyingi za seli. Kwa hiyo ukisema kansa ya ngozi bado haitoshi, inabidi ijulikane ni aina gani ya seli za ngozi zilizoathiriwa. Kwahiyo ngozi au ogani nyingine zinaweza kupata kansa za aina tofauti. Kuna Carcinomas, Sarcomas, Lymphomas, Leukemias nk. Na hizo aina pia zina aina zake tofautitofauti.

Bado!
Kuna kansa ambazo zina mahusiano na maambukizi ya aina fulani ya vimelea vya magonjwa, ingawa kansa nyingi haziambukizwi.

Sasa, kwanini nimeandika hivi?
Bila shaka umewahi kusikia huko mitaani habari za "DAWA YA KANSA" au Chanjo ya Kansa.

Sasa kwa elimu hiyo ndogo hapo juu, unadhani kuna dawa moja inaweza kutibu kansa zote hizo kwa pamoja?
Unaweza kuwa na funguo ya kuendesha magari yote ya Toyota na yote ya Nissan na yote ya Ford na yote ya Tesla na yote duniani?

Mganga wako wa kienyeji alikwambiwa anatibu kansa, ulimuuliza Kansa ipi?
Ulikuwa unajua Kansa sio ugonjwa mmoja?

Karibuni msosi.
Pombe Kistaarabu!
Sigara Acha!
Nawasilisha.
Dr. Chris Cyrilo.

KUNA NINI ZANZIBAR Nafuatilia kisa cha Haji Manara kishaa nawaza!Moja ya maukumu muhimu kwenye tasnia ya 'Intelligence' ...
22/02/2026

KUNA NINI ZANZIBAR
Nafuatilia kisa cha Haji Manara kishaa nawaza!
Moja ya maukumu muhimu kwenye tasnia ya 'Intelligence' ni kutumia taarifa za wazi ili kupata taarifa zilizofichwa. Unakusanya taarifa, unazifanyia upembuzi - unazitathmini na kuzichakata, halafu unapata 'taswira' ya taarifa zilizofichwa. Kisha unaweza kufanya uchunguzi ili kubaini ukweli usio na shaka.

Taarifa za wazi ni kwamba, Simba na Yanga zina mashabiki wengi kutoka Mikoa yote ya Tanzania na Zanzibar. Simba na Yanga, pamoja na kudhaminiwa na matajiri bado wanahitaji mapato kupitia tiketi za kutazama mechi zao. Mechi za ligi ya mabingwa Afrika na Mechi za Derby ndio mechi zenye mahudhurio na mapato makubwa. Mbali na mapato, Simba na Yanga bila shaka zinafanya kila liwezekanalo kuongeza mashwbiki, na kuwatunzana kuwafurahisha wale waliopo. Naam! Kitu kikubwa cha kuwapa mashabiki ni raha na furaha.
Bila shaka aya hiyo ya pili imenyooka, hakuna mawaa. Nimeandika mambo ya wazi kabisa ambayo kila mtu mzima anayafahamu.

Sasa, Kwanini Simba na Yanga wanapeleka mechi zao Zanzibar hata pale Uwanja wa Mkapa unapokuwa katika mazingira ya kuruhusu mchezo?
Je! Kuna taarifa gani ya siri ambayo inaweza kujibu swali hilo?
Wengine watasema ni maamuzi binafsi!
Wengine watasema Wanafuata bahati kwenye uwanja wa Amaan!
Wengine watasema wameagizwa na waganga wao!
Kila mtu anaweza kuwa na majibu yake.
Lakini maswali hayaishi.

Kwanini Simba na Yanga waache mapato makubwa Benjamin - Mkapa kwa ajili ya Zanzibar?
Kwanini Simba na Yanga wasumbue mashabiki kusafiri hadi Zanzibar, na kuwanyima mashabiki wengi zaidi fursa ya kutazama mchezo wao?
Kwanini Simba na Yanga watumie muda mrefu na nguvu kubwa kuvuka maji wakati makazi yao ni Dar es Salaam na kuna uwanja bora na mkubwa zaidi?
Kunani Zanzibar?

Je! Kuna makubaliano ya siri kati ya serikali ya Zanzibr na vilabu vya Simba na Yanga?
Je! Serikali ya Zanzibar inawalipa Simba na Yanga pesa kubwa kiasi cha wao kutojali mapato ya Benjamin Mkapa?
Je! Serikali ya Zanzibar inawalipa Simba na Yanga pesa ya kuwafanya waone mashabiki wao si kitu?

Je! Ni 'mpango wa siri' wa Serikali ya Zanzibar kuitangaza Zanzibar, kuchochea ukuaji wa michezo, buashara na utalii?

Cardinal Pengo, Gallery.
20/02/2026

Cardinal Pengo, Gallery.

Serikali ya CCM ilipoanza kupambana na wapinzani wake kwa kuwateka na kuwaua, tumelia  hadi macho yamevimba wakati wanaC...
19/02/2026

Serikali ya CCM ilipoanza kupambana na wapinzani wake kwa kuwateka na kuwaua, tumelia hadi macho yamevimba wakati wanaCCM wakitucheka na kutukebehi eti tunajiteka wenyewe!

Pamoja na vilio vyetu tulionya pia, kwamba uovu unaambukiza, uovu unasambaa, uovu ni kansa inayosambaa! Tulionya kwamba, WanaCCM pamoja na dharau zao na kejeli zao juu yetu sisi tunaotekwa na kuuawa, na wao pia hawapo salalama. Na kweli, ametekwa Waziri wa Zamani Ndg. Mwambe na kufanyiwa vitu vibaya, wapo mawaziri wengine wamewahi kuwekwa house arrest, na kwenye uchaguzi wao wa ndani wanafanyiana mambo haya na mengine ya ajabu. Hakuna aliye salama ndani ya uovu!

Tulionya tena, kwamba hao vijana wanaotumiwa kuteka na kuua wapinzani wataanza kutumia mbinu hizo kutafuta pesa. Kana kwamba watu hawa wanaotumiwa na baadhi ya viongozi wakisiasa na wale wa vyombo vya ulinzi na usalama wanaogopwa na hawaguswi, na kwakuwa wao ni sehemu ya ulinzi wa madaraka ya CCM basi hakuna kitu watafanywa na viongozi CCM. Tukio maaurufu la kuthibitisha madai haya ni tukio kutekwa na kupotezwa kwa baadhi ya wafanyabiashara wa Kariakoo, na jaribio la kutekwa mfanyabiashara Tarimo kule Kiluvya. Wahusika wa matukio haya wametajwa kuwa ni watumishi wa vyombo vya Ulinzi na Usalama.

Tulionya pia, kwakuwa serikali ya CCM imeruhusu matukio haya; kwanza kwa kutochukua hatua stahiki na pili kutoa kauli zinazochochea matukio haya (mfano, kauli kwamba hata nchi nyingine matukio haya yapo); basi tutarajie hata raia binafsi wenye roho chafu huko mitaani wakikosana wataanza kutekana na kuuana! Yes! Kwa sababu uovu, k**a ulivyo wema, unaambukiza, unasambaa!

Hata leo, wapo vijana ambao wanahisi matukio haya ni kwa watu fulani tu na wao hayawahusu! Nawajua vijana wa CCM wanaotukana wapinzani na wasiojali maovu wanaofanyiwa wakosoaji, wanaokejeli na kusema eti tunajiteka, nawajua ambao na wao yamewakuta. Waovu hawa, wameruhusiwa na serikali ya CCM, lakini uovu wao utawaumiza wote wakiwemo hao walioruhusu!

Shetani limeshika hatamu, Shetani halishibi damu.
Nawasilisha.
Dr. Chris Cyrilo.
--------------------------
Usikose kusoma kitabu cha ISTILAHI ZA UHALIFU NA USALAMA popote Tanzania.
Nicheki kwa 0713933736 / 0745830775

17/02/2026

VIDEO
Msikilize Mtanzania aliye vitani huko Urusi akitoa maelezo yake juu ya hali ilivyo. Tofauti na wengine, yeye anaonekana yupo salama, na hajutii kuwa huko.
Huyu hajakutana na maguruneti au mwenetu anatuita tukaumie wote?

Zingatia! Warusi hawataki kupoteza nguvu zao, wanataka kubaki kuwa super power. Mapema kabisa walipoona mataifa ya magharibi yanamimina silaha kusaidia Ukraine, Warusi walibadili mbinu haraka; moja kutumia silaha za gharama nafuu kutoka Iran, Korea Kaskazini, ili kulinda silaha kali za gharama kubwa, na pili kutumia mamluki (mercenaries) mfano; Wagner Group na wanadamu wengine kutoka kokote duniani wanaoweza kupigana kwa ajili ya ujira. Lengo ni kulinda idadi ya askari wao raia wa Urusi.

Funzo; usitumie nguvu kubwa kupambana na adui mdogo wakati kuna maadui wakubwa zaidi wanakutamani. Ni funzo la kijeshi na maisha pia.

Msikilize mwamba! Anawaita! Halafu huyu mwanangu wa Tanga kabisa mitaa ya Majani Mapana!
Maisha ni nini?
Oyaa! Anayetaka kwenda Urusi au Ukraine anicheki tuongee atanilipa ngapi? đŸ˜‚

Nawasilisha!
Dr. Chris Cyrilo.

Namuonea huruma!
16/02/2026

Namuonea huruma!

16/02/2026

VIDEO; UTEKAJI MUHEZA.
Kuhusu watekaji na wauaji!
Kwanza, namuonea huruma huyu jamaa anaelekeza malalamiko yake kwa watu walewale!

Pili, niliwahi kuandika madhara ya serikali za vyama tawala kutumia makundi ya watekaji na wauaji ili kukandamiza upinzani; madhara ambayo kila mtu anaweza kuyaona ni serikali kukosa uhalali wa kuongoza raia, na raia kuichukia serikali na kutengeneza uadua mkali kati ya raia na viongozi wa serikali. Hilo linaonekana kirahisi lakini watekelezaji wa matukio haya hawajali kwa sababu kipaumbele chao sio ustawi wa taifa moja lenye amani na utulivu, kipaumbele chao ni kushikilia madaraka ili waendelee kutapanya mali za umma kwa gharama za damu za wapinzani.

Sasa kuna madhara ambayo si rahisi kuyaona;
Moja, ni wale vijana wanaotumiwa kuteka na kuua wapinzani wanapoanza kufanya matukio hayo bila kutumwa. Kwa kuwa wana silaha na kwa kuwa ni marafiki wa wenye madaraka katika uhalifu, basi hakuna wa kuwagusa wanapoteka mfanyabiashara, kupora pesa zake na kumuua, halafu wanasingizia siasa.
Pili, ndani ya serikali, viongozi wa ngazi tofauti wa kisiasa na wale wa vyombo vinavyoitwa vya ulinzi na usalama, na marafiki zao kujiundia magenge ya uhalifu kwa ajili ya manufaa yao ya kisiasa na kibiashara. Na kwakuwa serikali tayari ilishabaliki matukio haya, nani wa kumnyooshea mwenzia kidole?
Viongozi wa kisiasa na wale wa vyombo vya ulinzi; wakuu wa mikoa na wilaya, mawaziri, ma RPC na ZCO, wakimiliki magenge ya uhalifu ya kuteka na kuua watu nani atakayemkemea mwingine?

Unajikuta kwenya hatari ya kutekwa na genge la kiongozi mmoja, unapeleka malalamiko yako kwa kiongozi mwenye genge kubwa na katili zaidi! Unahisi kuna usalama? Ole wako magenge hayo yanashirikiana.

Walianza kwa upinzani, wakakubaliana hiyo ndio mbinu ya kushikilia madaraka, wamenogewa, sasa wanatumia mbinu hizo kwenye kufanya mambo yao binafsi.
Mbegu imechepua!
Jiti limemea!
Matunda tutakula!
Matunda machungu! Mabaya! Ufala
Nchi yenye ufala!

Shetani limevimbiwa damu!
Shetani litatapika damu!
Nawasilisha
Dr. Chris Cyrilo.

15/02/2026

VIDEO
Mtoto "muhaini aliyechoma vituo vya mafuta" akisimulia alivyopigwa risasi Oktoba 29.

Shetani limevimbiwa damu!
Shetani litatapika damu!
Nawasilisha.
Dr. Chris Cyrilo.

Yes! Ni upumbavu.
02/02/2026

Yes! Ni upumbavu.

Address

Zip Code 00083
Dar Es Salaam

Telephone

+255713933736

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Dr. Christopher Cyrilo posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Dr. Christopher Cyrilo:

Shortcuts

Share

Category