14/07/2026
SABABU ZA FIGO KUHARIBIKA AU KUFELI
• Kisukari kisichodhibitiwa vizuri
• Shinikizo la damu la muda mrefu
• Maambukizi ya njia ya mkojo (UTI) yanayoenea hadi kwenye figo
• Kutumia dawa za maumivu (painkillers) mara kwa mara bila ushauri wa daktari
• Kunywa maji kwa kiwango kidogo kwa muda mrefu
• Mawe kwenye figo yanayoziba njia ya mkojo
• Magonjwa ya kurithi yanayoathiri figo
• Kuvuta sigara
• Magonjwa ya kinga ya mwili yanayoshambulia figo (k**a lupus)
• Kuziba kwa njia ya mkojo kutokana na tezi dume kuongezeka au sababu nyingine
Linda afya ya figo zako kwa kufanya uchunguzi wa afya mara kwa mara, kudhibiti kisukari na shinikizo la damu, na kutafuta matibabu mapema unapopata maambukizi ya njia ya mkojo au dalili nyingine zinazohusiana na figo.