Taasisi ya Tiba ya Mifupa - MOI

Taasisi ya Tiba ya Mifupa - MOI Tunatoa matibabu ya Kibingwa na bobezi ya Mifupa, Upasuaji wa Ubongo,Mgongo, Mishipa ya fahamu, huduma za dharura na ajali

The Muhimbili Orthopaedic Institute (MOI) is an autonomous Institution established through an Act of Parliament No 7 of 1996 with the main objective of providing primary,secondary and Tertiary care for preventive and curative health services in the field of Orthopaedic,Traumatology and neurosurgery
The management of the Institute is based on Public/Private Mix concept geared towards performance improvement and and self sustainability.

WATUMISHI PSSSF WACHANGIA MILIONI 10 KWA MATIBABU YA WATOTO WENYE VICHWA VIKUBWA NA MGONGO WAZI MOINa Amani Nsello - MOI...
04/06/2026

WATUMISHI PSSSF WACHANGIA MILIONI 10 KWA MATIBABU YA WATOTO WENYE VICHWA VIKUBWA NA MGONGO WAZI MOI

Na Amani Nsello - MOI

Watumishi wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) wamechangia kiasi cha shilingi milioni 10 kusaidia matibabu ya watoto wenye tatizo la vichwa vikubwa na mgongo wazi wanaopatiwa matibabu katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI).

Mbali na mchango huo wa fedha, watumishi hao pia walikabidhi msaada wa mahitaji mbalimbali muhimu kwa watoto hao, ikiwemo miswaki, sabuni za unga, pampasi na maziwa, ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za kuboresha ustawi wao wakati wa matibabu.

Akizungumza wakati wa kukabidhi msaada huo jana Juni 03, 2026, Mratibu wa shughuli hiyo kutoka PSSSF, Bi. Maria Lupondo, amesema watumishi wa mfuko huo wameguswa na mahitaji ya watoto hao na kuona umuhimu wa kushiriki katika kuwasaidia ili kupunguza changamoto wanazokutana nazo wao na familia zao.

"Mchango huu unaakisi dhamira ya watumishi wa PSSSF ya kurejesha sehemu ya mafanikio yetu kwa jamii kwa kuwasaidia wenye uhitaji, hususani watoto wanaohitaji huduma maalumu za matibabu".

Kwa upande wake, Meneja wa Wagonjwa wa Ndani MOI, Magreth Kumpuni, ambaye alipokea msaada huo kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo, aliwashukuru watumishi wa PSSSF kwa moyo wao wa kujitolea na msaada walioutoa.

Amesema mchango huo utasaidia kuboresha huduma na mahitaji ya watoto wanaopatiwa matibabu katika taasisi hiyo, huku akizitaka taasisi na wadau wengine kuendelea kushirikiana na MOI katika kusaidia makundi yenye mahitaji maalumu ya kiafya.

Msaada huo ni sehemu ya juhudi za wadau mbalimbali zinazolenga kuimarisha huduma za afya na kuwapatia matumaini watoto wanaokabiliwa na changamoto za vichwa vikubwa na mgongo wazi nchini.

WAUGUZI MOI WAPATIWA MAFUNZO YA KUJIKINGA NA MAGONJWA HATARI YA KUAMBUKIZANa Amani Nsello- MOIKufuatia uwepo wa ugonjwa ...
03/06/2026

WAUGUZI MOI WAPATIWA MAFUNZO YA KUJIKINGA NA MAGONJWA HATARI YA KUAMBUKIZA

Na Amani Nsello- MOI

Kufuatia uwepo wa ugonjwa hatari wa Ebola katika nchi jirani za Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na Uganda, wauguzi wa Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI) wamepatiwa mafunzo maalum ya kujikinga dhidi ya maambukizi kwa kutumia afua za kukinga na kudhibiti maambukizi.

Mafunzo hayo yaliandaliwa na Kitengo cha Ukaguzi wa Kitabibu na Udhibiti wa Ubora wa Huduma kwa kushirikiana na Timu ya Maandalizi ya Kukabiliana na Magonjwa Hatari, ambapo washiriki walipatiwa mafunzo ya nadharia na vitendo kuhusu mbinu bora za kujikinga na maambukizi.

Akizungumza leo Jumatano Juni 03, 2026 wakati wa mafunzo hayo, Muuguzi Mwandamizi na Mkufunzi wa Dhana za Kukinga na Kudhibiti Maambukizi, BiGrace Ngugo, amesema:

"Silaha pekee ya kukabiliana na adui huyu hatari ni kuhakikisha watumishi wa afya wanafuata miongozo ya kukinga na kudhibiti maambukizi muda wote wanapokuwa katika utekelezaji wa majukumu yao."

Kwa upande wake, Bi. Zaituni Bembe amesema Ni muhimu kuendelea kuwa tayari wakati wote kwa kuhakikisha taratibu za kukinga na kudhibiti maambukizi zinafuatwa kikamilifu ili kuzuia kuenea kwa ugonjwa endapo atapatikana mshukiwa au mgonjwa.

Mafunzo hayo ni sehemu ya mikakati ya MOI ya kuimarisha utayari wa watumishi wa afya katika kukabiliana na magonjwa hatari ya kuambukiza na kuhakikisha usalama wa wagonjwa, watumishi pamoja na jamii kwa ujumla.

30/05/2026
30/05/2026

JK AKUTANA NA BI. CATHERINE P. CONRAD MINJA, NI MSICHANA ALIYEFANYIWA UPASUAJI WA MOYO KWA MAFANIKIO KATIKA TAASISI YA MIFUPA YA MUHIMBILI (MOI) MIAKA 18 ILIYOPITA.

Asubuhi ya Ijumaa, Novemba 14, 2008 Rais wa Awamu ya Nne wa Tanzania, Mhe. Dkt Jakaya Mrisho Kikwete, alisimama kwa muda kando ya kitanda cha binti mdogo Catherine P. Conrdad Minja mwenye umri wa miaka minne katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI) akimsabahi na kumtakia nafuu ya haraka baada ya kufanyiwa upasuaji wa moyo mapema wiki hiyo, akiwa mmoja wa wagonjwa wa mwanzo kufanyiwa upasuaji huo katika Taasisi hiyo.

Jioni ya Ijumaa Mei 29, 2026 - yaani jana - Rais huyo mstaafu wa Awamu ya Nne wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete amekutana kwa mara nyingine na Catherine P. Conrad Minja ambaye Julai 19 mwaka huu atatimiza umri wa miaka 22 , ikiwa ni miaka 18 toka walipoonana MOI baada ya kufanyiwa upasuaji wa moyo mapema wiki hiyo.

Catherine hivi sasa ni mwanafunzi wa mwaka wa kwanza akisomea udaktari katika Chuo Kikuu cha Kairuki jijini Dar es salaam, alifika ofisini kwa Rais Mstaafu kumsabahi na kumshukuru kwa juhudi zake za kuanzisha na kusimamia taasisi za magonjwa ya moyo.

Dkt. Kikwete amempongeza Catherine kwa kuchagua masomo ya udaktari k**a alivyomuahidi miaka 18 iliyopita, na amefurahi kumuona mmoja wa wagonjwa wa kwanza kufanyiwa upasuaji Taasisi ya MOI ambayo ni moja ya taasisi za rufaa zinazoongoza Afrika Mashariki katika kushughulikia kesi ngumu za magonjwa na majeraha ya mifupa, misuli, viungo, ubongo na mfumo wa fahamu.

Catherine amemwambia Rais Mstaafu kwamba angependa kuwa Daktari Bingwa wa magonjwa ya moyo huko mbeleni, ili asaidie watu wenye shida hiyo iwe k**a shukrani zake kwa Mungu kwa kuwezesha apone na kuendelea kuishi.

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA  AIPONGEZA MOI KUSOGEZA HUDUMA ZA KIBINGWA MBEYANa Abdallah Nassoro - MbeyaNaibu Waz...
30/05/2026

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA AIPONGEZA MOI KUSOGEZA HUDUMA ZA KIBINGWA MBEYA

Na Abdallah Nassoro - Mbeya

Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Denis Londo ametembelea banda la Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI) na kupongeza juhudi zinazofanywa na taasisi hiyo katika kusogeza huduma za kibingwa na kibobezi za Mifupa na Ubongo karibu na wananchi wa Mbeya.

Mhe. Londo ametembelea banda hilo leo Mei, 30, 2026 katika maonesho ya Nne ya Mbeya City Expo 2026 katika viwanja vya Uhindini Jijini Mbeya.

"Hongereni sana Kwa kusogeza huduma za kibingwa na kibobezi kwa wananchi wa Mbeya, huduma zenu ni muhimu katika ustawi wa jamii yetu, endeleeni kuwatumikia watanzania" amesema Mhe. Londo

Kwa upande wake daktari bingwa wa radiolojia kutoka MOI Dr. Vaileth Kalinga amemweleza Naibu Waziri huyo kuwa taasisi hiyo imefanikiwa kupunguza idadi ya wagonjwa wanaopewa rufaa kwenda nchi za nje Kwa matibabu kwa kuanzisha huduma mpya muhimu.

Ametaja baadhi ya huduma hizo kuwa ni pamoja na matibabu ya kichwa kikubwa na mgongo wazi, urekebishaji wa kibiongo na matibabu ya kiharusi.

"Kwa sasa matibabu ya magonjwa kichwa kikubwa na mgongo wazi, kibiongo pamoja na kiharusi yanafanyika MOI, zamani ilikuwa wanapewa rufaa kwenda kutibiwa nje ya nchi" amesema Dr. Vaileth

Maonesho ya Mbeya City Expo 2026, yanafikia tamati leo Mei, 30, 2026 ambapo taasisi ya MOI imetoa huduma kwa wagonjwa zaidi ya 300.

MKUU WA WILAYA KILOMBERO AHITIMISHA KAMBI YA MATIBABU YA MOI; ZAIDI YA WAGONJWA 1,000 WAPATIWA HUDUMANa Erick Dilli- KIL...
30/05/2026

MKUU WA WILAYA KILOMBERO AHITIMISHA KAMBI YA MATIBABU YA MOI; ZAIDI YA WAGONJWA 1,000 WAPATIWA HUDUMA

Na Erick Dilli- KILOMBERO

Mkuu wa Wilaya ya Kilombero, Mhe. Dunstan Kyobya, amehitimisha rasmi kambi ya matibabu iliyoandaliwa na Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI) katika Halmashauri ya Ifakara, ambapo zaidi ya wagonjwa 1,000 wamepatiwa huduma mbalimbali za matibabu.

Kambi hiyo imehitimishwa leo, Mei 29, 2026, katika Hospitali ya Rufaa ya St. Francis iliyopo Halmashauri ya Ifakara.

Akizungumza wakati wa hafla ya hitimisho, Mhe. Kyobya ameushukuru uongozi wa MOI kwa kupeleka huduma hizo karibu na wananchi wa Wilaya ya Kilombero na maeneo ya jirani, hatua iliyowezesha wananchi wengi kupata matibabu ya kibingwa bila kusafiri umbali mrefu.

“Niwashukuru Madaktari Bingwa pamoja na watumishi wote kutoka MOI mliofika katika kambi hii, kwani uwepo wenu umeleta hatua kubwa katika matibabu ya magonjwa ya mifupa, ubongo, mgongo na mishipa ya fahamu,” amesema Mhe. Kyobya.

Aidha, amepongeza moyo wa kujitolea ulioonyeshwa na wataalamu hao kwa kuwahudumia wananchi hata nje ya muda rasmi wa kazi.

“Niwashukuru kwa kujitoa kwenu na kuwahudumia wananchi hawa hata nje ya muda wa kazi. Hii inaonyesha moyo wenu mzuri na dhamira ya kweli ya kuwahudumia Watanzania,” ameongeza.

Kwa upande wake, Meneja wa Huduma za Utengamao wa MOI, Bi. Marry Chandeu, ameishukuru Ofisi ya Mkuu wa Wilaya pamoja na uongozi wa Hospitali ya St. Francis kwa ushirikiano na mapokezi mazuri waliyopewa katika kipindi chote cha kambi hiyo.

Bi. Chandeu amesema wataalamu hao wamebaini changamoto mbalimbali za kiafya kwa wananchi waliojitokeza kupata huduma, hususan magonjwa ya mifupa, ubongo na mgongo kwa watu wazima.

“Katika idadi ya wagonjwa tuliowaona, wengi walikuwa na magonjwa ya mifupa, ubongo na mgongo kwa watu wazima. Kwa watoto, tumeona dalili kubwa za kichwa kikubwa na mgongo wazi. Hivyo, k**a wataalamu tumetoa tiba pamoja na elimu ya namna ya kukabiliana na changamoto hizo,” amesema Bi. Chandeu.

Naye Mkurugenzi wa Tiba wa Hospitali ya St. Francis, Father Dkt. Winfrid Gingo, ameishukuru MOI kwa kuandaa kambi hiyo hospitalini hapo, akibainisha kuwa mbali na wananchi kupata hudum

TIMU YA MADAKTARI KUTOKA CHINA KUSHIRIKIANA NA MOI KUIMARISHA HUDUMA ZA KIBINGWA Timu ya Madaktari kutoka China leo Mei,...
28/05/2026

TIMU YA MADAKTARI KUTOKA CHINA KUSHIRIKIANA NA MOI KUIMARISHA HUDUMA ZA KIBINGWA

Timu ya Madaktari kutoka China leo Mei, 28, 2026 imeshirikiana na wataalamu wa Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI) kutoa huduma za kibingwa za upasuaji wa ubongo kwa teknolojia ya kisasa uliofanyika kwa mafanikio makubwa katika taasisi hiyo.

Timu hiyo imeambatana na waandishi wa habari kutoka shirika la habari nchini humo ( Xinhua News Agency) wanaorekodi baadhi ya matukio hospitalini hapo kwa ajili ya kuandaa video maalum itakayoonesha ushirikiano wa huduma za afya, ubadilishanaji wa uzoefu wa kitabibu pamoja na mafanikio ya huduma zinazotolewa MOI.

DC KYOBYA AISHUKURU MOI KUWEKA KAMBI YA MATIBABU WILAYANI KILOMBERONa Erick Dilli - KilomberoMkuu wa Wilaya ya Kilombero...
27/05/2026

DC KYOBYA AISHUKURU MOI KUWEKA KAMBI YA MATIBABU WILAYANI KILOMBERO

Na Erick Dilli - Kilombero

Mkuu wa Wilaya ya Kilombero, Mhe. Wakili Dunstan Kyobya, ameishukuru Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI) kwa kupeleka huduma za kibingwa za matibabu ya Mifupa, Ubongo, Mgongo na Mishipa ya Fahamu katika Halmashauri ya Ifakara mkoani Morogoro.

Pongezi hizo amezitoa leo Mei 27, 2026, alipokutana na wataalam wa MOI katika ofisi yake na kupongeza uamuzi wa kusogeza huduma karibu na wananchi kupitia kambi maalum inayofanyika katika Hospitali ya Rufaa ya Mtakatifu St. Francis, Ifakara.

“Niwapongeze MOI kwa matibabu bora ya kibingwa ya mifupa, mgongo na mishipa ya fahamu mnayotoa kwa Watanzania. Mimi mwenyewe nilipata ajali na nikapatiwa matibabu MOI, na mpaka sasa naendelea vizuri. Pia niwashukuru kwa kusogeza huduma hizi karibu na wakazi wa Kilombero, hakika wananchi wanafarijika,” amesema Mhe. Kyobya.

Kwa upande wake, Daktari Bingwa wa Mifupa kutoka MOI, Dkt. Allen Kissanga, amemshukuru Mkuu wa Wilaya kwa mapokezi mazuri na kuahidi kuendelea kutoa huduma kwa wananchi wengi zaidi wa Wilaya ya Kilombero na maeneo jirani hadi mwisho wa kambi hiyo.

Naye Mkuu wa Idara ya Mifupa katika Hospitali ya St. Francis, Dkt. Ombeni Bill, amesema hospitali hiyo itaendelea kushirikiana na watumishi wa MOI ili kuhakikisha huduma zinatolewa kwa ufanisi kwa wananchi wanaohitaji matibabu.

Kambi hiyo ya matibabu inaendelea katika Hospitali ya Rufaa ya St. Francis, Ifakara, ambapo huduma zinazotolewa ni pamoja na uchunguzi na matibabu ya Mifupa, Ubongo, Mgongo na Mishipa ya Fahamu, magonjwa ya ndani, mazoezi tiba, huduma za dawa, elimu ya tiba lishe pamoja na huduma za viungo bandia.

DC KYOBA AISHUKURU MOI KUWEKA KAMBI YA MATIBABU WILAYANI KILOMBERONa Erick Dilli - KilomberoMkuu wa Wilaya ya Kilombero,...
27/05/2026

DC KYOBA AISHUKURU MOI KUWEKA KAMBI YA MATIBABU WILAYANI KILOMBERO

Na Erick Dilli - Kilombero

Mkuu wa Wilaya ya Kilombero, Mhe. Wakili Dunstan Kyobya, ameishukuru Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI) kwa kupeleka huduma za kibingwa za matibabu ya Mifupa, Ubongo, Mgongo na Mishipa ya Fahamu katika Halmashauri ya Ifakara mkoani Morogoro.

Pongezi hizo amezitoa leo Mei 27, 2026, alipokutana na wataalam wa MOI katika ofisi yake na kupongeza uamuzi wa kusogeza huduma karibu na wananchi kupitia kambi maalum inayofanyika katika Hospitali ya Rufaa ya Mtakatifu St. Francis, Ifakara.

“Niwapongeze MOI kwa matibabu bora ya kibingwa ya mifupa, mgongo na mishipa ya fahamu mnayotoa kwa Watanzania. Mimi mwenyewe nilipata ajali na nikapatiwa matibabu MOI, na mpaka sasa naendelea vizuri. Pia niwashukuru kwa kusogeza huduma hizi karibu na wakazi wa Kilombero, hakika wananchi wanafarijika,” amesema Mhe. Kyobya.

Kwa upande wake, Daktari Bingwa wa Mifupa kutoka MOI, Dkt. Allen Kissanga, amemshukuru Mkuu wa Wilaya kwa mapokezi mazuri na kuahidi kuendelea kutoa huduma kwa wananchi wengi zaidi wa Wilaya ya Kilombero na maeneo jirani hadi mwisho wa kambi hiyo.

Naye Mkuu wa Idara ya Mifupa katika Hospitali ya St. Francis, Dkt. Ombeni Bill, amesema hospitali hiyo itaendelea kushirikiana na watumishi wa MOI ili kuhakikisha huduma zinatolewa kwa ufanisi kwa wananchi wanaohitaji matibabu.

Kambi hiyo ya matibabu inaendelea katika Hospitali ya Rufaa ya St. Francis, Ifakara, ambapo huduma zinazotolewa ni pamoja na uchunguzi na matibabu ya Mifupa, Ubongo, Mgongo na Mishipa ya Fahamu, magonjwa ya ndani, mazoezi tiba, huduma za dawa, elimu ya tiba lishe pamoja na huduma za viungo bandia.

Tunawatakia Waislamu na Watanzania wote Heri ya Sikukuu ya Eid Al Adha Mubarak Mei 27, 2026
27/05/2026

Tunawatakia Waislamu na Watanzania wote Heri ya Sikukuu ya Eid Al Adha Mubarak Mei 27, 2026

Address

P. O. BOX 65474
Dar Es Salam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Taasisi ya Tiba ya Mifupa - MOI posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Taasisi ya Tiba ya Mifupa - MOI:

Shortcuts

Share

Category