03/08/2026
JINI MAHABA (SPIRITUAL HUSBAND OR WIFE) PART 1
Huyu ni jini mshenzi mwenye kuangamiza maisha ya watu wengi sana, leo mamilioni ya watu duniani wanaishi maisha ambayo si yao kwasababu ya huyu kiumbe, tambua kuwa Spiritual husband (mume wa kiroho) au spiritual wife (mke wa kiroho) ni kiumbe wa ulimwengu wa roho ambaye amejifungamanisha na mtu kana kwamba ni mwenzi wake wa ndoa.
Wakati mwingine kiumbe huyo humvaa mtu tangu akiwa mtoto na hukua nae mpaka anaingia utu uzima, anakuwa anakujua nje ndani, anajua kila kitu kuhusu wewe, anajua udhaifu wako na uimara wako uko wapi, huyu kumuepuka sio jambo la mchezo, unahitaji kujitoa zaidi ya unavyoweza kufikiria, ana uwezo wa kukushawishi ufanye mambo fulani kwa kukuwekea mitego kulingana na jinsi anavyokujua kitabia na akafanikiwa kukuingiza kwenye mtego.
Huyu anayekuingia ukiwa mtoto mara nyingi ni wa kutoka kwenye generation ya ukoo wako, ni spirits za kutoka kwenu eidha umamani au ubabani,
Na wengi wameona ni ngumu kumtoa na kumuepuka wakaamua kuungana nae, yaani wakaamua kumkubali na kuishi nae kwa makubaliano, naposema makubaliano namaanisha unaingia nae makubaliano kwamba akuache huru katika jambo hili na lile na wewe utamuacha huru katika jambo hili na lile, lakini si kila mtu anaweza kukubaliana nae ndio hapo linapokuja swala la kupambana ili kuhakikisha unamuepuka na kuishi huru kwenye maisha yako.
Huyu ukishindwa kumdhibiti, ukawa wa kutumia dawa kwa mzaha au unafanya maombi kwa mzaha, unatumia dawa baadae unachoka unaacha, unafanya maombi unachoka unaacha, yaani ile hali ya kujidanganya au kudanganywa utatumia dawa siku chache eti umemaliza, aloo pole sana maana cha moto utakiona, maana unakuwa umeingia nae kwenye vita, atahakikisha maisha yako yanakuwa zaidi ya jehanamu katika kila eneo.
Kiumbe huyu huweza kuonyesha wivu kwa mahusiano ya mtu, hivyo atasababisha migogoro ya kimapenzi, kuvunjika au kuwafanya watu wasioe wala kuolewa kabisa.
Amini usiamini kuna watu wengi sana wanaishi na kiumbe huyu na maisha yao ya mahusiano ni k**a hadithi fulani ya kustaajabisha.
Dalili za kuwa una kiumbe huyu nimeshazieleza kwenye video zilizopita, nitaendelea kuleta masomo mengine zaidi kumuhusu.
Hii ni sehemu ya kwanza, sehemu ya pili itakujia na nitaeleza dawa mbali mbali ambazo unaweza kuwa unatumia ili kuendelea kutafuta nusura na hatimaye uwe huru na maisha yako.
Usiache ku-share sadaka hii kwa wengine.
Asanteni sana.
Welcome Halisi Naturalist Tanzania a trusted source for herbal medicine and natural health education. Learn how to heal and restore your body naturally with proven remedies. πΏ
Whatsapp +255788900445
πGeita, Dar es salaam Tanzania