TFNC Tanzania

TFNC Tanzania Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from TFNC Tanzania, Nutritionist, Ilala.

TAMISEMI  YAIUNGA MKONO TFNC KUELEKEA  UTEKELEZAJI WA MRADI WA IMAN AWAMU YA PILI Dodoma, Juni 12, 2026 Timu ya wataalam...
12/06/2026

TAMISEMI YAIUNGA MKONO TFNC KUELEKEA UTEKELEZAJI WA MRADI WA IMAN AWAMU YA PILI

Dodoma, Juni 12, 2026

Timu ya wataalamu kutoka Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC) pamoja na wadau wa Mradi wa IMAN II (Lishe Yangu), leo imekutana na viongozi wa Ofisi ya Waziri – TAMISEMI mjini Dodoma kwa lengo la kujadili mikakati ya utekelezaji wa mradi huo unaolenga kuboresha lishe kwa wanawake wajawazito nchini.

Kikao hicho kimeongozwa na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii, Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI, Dkt. Paul Chaote , na kuhudhuriwa na Wataalamu kutoka Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC) na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) wakiongozwa na Msimamizi wa Shughuli za Lishe nchini kutoka Shirika hilo Bwa. Patrick Codjia na maafisa wengine kutoka TAMISEMI.

Katika kikao hicho, washiriki wamejadili hatua mbalimbali za utekelezaji wa mradi, ikiwa ni pamoja na maandalizi ya uzinduzi rasmi wa IMAN II na namna ya kuwafikia walengwa ili kuhakikisha mradi huo unatekelezwa kwa ufanisi.

Dkt Chaote amesisitiza ushirikiano wa karibu kati ya TFNC, TAMISEMI na UNICEF katika utekelezaji wa mradi huo ili kuleta matokeo chanya yatakayosaidia kuboresha afya na lishe ya wanawake wajawazito nchini.

Uzinduzi rasmi wa mradi huo unatarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwezi Juni, 2026 katika Mkoa wa Njombe, ambapo wadau mbalimbali wa sekta ya afya na lishe wanatarajiwa kushiriki.

*TFNC YATAMBULISHA AWAMU YA PILI YA MRADI WA KUBORESHA LISHE KWA WANAWAKE WAJAWAZITO (IMAN II)*DODOMA – Serikali kupitia...
11/06/2026

*TFNC YATAMBULISHA AWAMU YA PILI YA MRADI WA KUBORESHA LISHE KWA WANAWAKE WAJAWAZITO (IMAN II)*

DODOMA – Serikali kupitia Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC), kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo, imetambulisha rasmi awamu ya pili ya mradi wa kuboresha lishe kwa wanawake wajawazito unaojulikana k**a “Lishe Yangu” (IMAN II).

Mradi huo unalenga kupunguza changamoto za lishe na kuhakikisha wajawazito wanapata virutubishi muhimu katika kipindi chote cha ujauzito.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa kikao kazi cha kujadili mradi huo leo tarehe 11 Juni 2026 katika Ukumbi wa St. Gaspar jijini Dodoma, Mkurugenzi wa Idara ya Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu-TAMISEMI, Dkt. Rashid Mfaume, ameipongeza TFNC na wadau wote kwa hatua hiyo.

Dkt. Mfaume ameahidi kuwa serikali kupitia Wizara ya Afya na TAMISEMI itaendelea kutoa ushirikiano wa karibu ili kufanikisha utekelezaji wa mradi huo katika maeneo yote yaliyokusudiwa.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa TFNC, Dkt. Germana Leyna, amebainisha kuwa mradi huu awamu hii umeelekezwa zaidi katika mikoa minne ambayo ni Dodoma, Njombe, Mbeya, na Songwe.

Dkt.Germana amesema uzinduzi rasmi wa mradi wa IMAN unatarajiwa kufanyika mkoani Njombe ifikapo mwishoni mwa mwezi huu wa Juni, 2026.

Mradi wa “Lishe Yangu” unatekelezwa chini ya ufadhili wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF). Lengo kuu ni kuboresha lishe ya mama na mtoto kwa kuhamasisha utekelezaji wa kitita cha huduma muhimu za lishe.

Kupitia afua za mradi huu, wanawake wajawazito watawezeshwa kupata huduma bora za lishe ili kupunguza tatizo la upungufu wa virutubishi mwilini (micronutrient deficiency), kuboresha afya zao wakati wa ujauzito, na kuweka msingi imara wa ukuaji wa mtoto aliye tumboni.

Kikao kazi hicho kimehudhuriwa na wadau mbalimbali muhimu, wakiwemo Maafisa Lishe kutoka mikoa ya Dodoma, Njombe, Mbeya na Songwe, wawakilishi kutoka Bohari ya Dawa (MSD), Mfamasia Mkuu, na viongozi kutoka Wizara ya Afya na Ofisi ya Waziri Mkuu.

We are thrilled to announce that the Tanzania Food and Nutrition Centre (TFNC) is the Key Supporting Partner for the 3rd...
11/06/2026

We are thrilled to announce that the Tanzania Food and Nutrition Centre (TFNC) is the Key Supporting Partner for the 3rd Future Food Livestock & Poultry Expo 2026! 🤝🌾

Join industry leaders, innovators, and policymakers as we collaborate to shape the future of food security, livestock, and poultry production across Africa. 📈

📅 Date: 2nd - 3rd September 2026

📍 Venue: Mwalimu J.K. Nyerere Trade Fair Grounds, Dar es Salaam, Tanzania

🌐 Register today: www.worldagrifood.com

11/06/2026

📍 Fursa ya Mafunzo ya Muda Mfupi: Usindikaji wa Unga Mchanganyiko

Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC) inakaribisha wajasiriamali wote wanaosindika vyakula vya watoto (miezi 6–23) kwenye mafunzo maalum ya nadharia na vitendo.

📚 Mada zitakazofundishwa:
* Masuala ya msingi ya chakula cha nyongeza cha watoto.
* Uongezaji wa virutubisho na kanuni bora za usindikaji.
* Mbinu za kupunguza sumu kuvu na kuzuia vimelea.

🗓 Tarehe: 25 - 26 Juni, 2026
💰 Ada: TSh 160,000/= (Inajumuisha chakula, ukumbi na cheti)

📍 Mahali: TFNC - Mikocheni (Sembeti St.)

✍️ Sifa ya Muombaji: Uwezo wa kusoma na kuandika.

Nenda kwenye tovuti yao au skani QR kodi iliyopo kwenye picha ili kujisajili sasa! Wahi nafasi yako.

📢 WITO KWA WADAU WA URUTUBISHAJI CHAKULA!Ili kufikia malengo ya utekelezaji wa afua za urutubishaji wa chakula nchini, W...
10/06/2026

📢 WITO KWA WADAU WA URUTUBISHAJI CHAKULA!

Ili kufikia malengo ya utekelezaji wa afua za urutubishaji wa chakula nchini, Wito umetolewa kwa wadau wa Uongezaji wa Virutubishi kwenye Vyakula nchini, kuitumia kikamilifu Maabara ya Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC) katika kuboresha mbinu mbalimbali katika utekelezaji wa afua za urutubishaji wa vyakula nchini.

Akitoa Salama za Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzani (TFNC) katika Mkutano wa 40 wa Jukwaa la Wadau wa Urutubishaji nchini, kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Sayansi ya Chakula na Lishe Bw. Tedson Lukindo, amesema Milango ya Taasisi iko wazi kwa wadau wote kushirikiana na Taasisi katika utekelezaji wa afua mbalimbali za kilishe ikiwemo eneo la Urutubishaji.

Lukindo amesema Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania imeendelea na itaendelea kutoa ushirikiano kwa wadau mbalimbali katika utekelezaji wa shughuli za kilishe nchini.

🍏 Leo ni Siku ya Usalama wa Chakula Duniani! 🌍Chakula salama ni msingi wa afya bora na maisha marefu. Usalama wa chakula...
07/06/2026

🍏 Leo ni Siku ya Usalama wa Chakula Duniani! 🌍

Chakula salama ni msingi wa afya bora na maisha marefu. Usalama wa chakula unaanza na mimi na wewe—tangu sokoni, jikoni, hadi mezani. Hakikisha unachokula leo kiko salama! 🍽️✨

06/06/2026

Ujumbe kutoka kwa Afisa Lishe Mtafiti Jubilate Mremi, kuelekea Siku ya Chakula Salama Duniani.

04/06/2026

Mafunzo ya TFNC Yamwongezea Uwezo Mjasiriamali wa Unga Mchanganyiko Njombe

Mjasiriamali anayejishughulisha na uandaaji wa unga mchanganyiko kutoka Njombe, Bwa. Richard Mgaya, amepongeza mafunzo ya Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC). Mgaya ameeleza kuwa mafunzo hayo yanaenda kuongeza uwezo wake wa kuzalisha bidhaa bora, salama, na zinazokidhi viwango vinavyotakiwa kwa afya ya watumiaji.

Mgaya ameyasema hayo baada ya kukamilisha mafunzo hayo maalumu ya siku tano ya uandaaji wa unga mchanganyiko yaliyotolewa na TFNC, yakilenga kuwajengea uwezo wajasiriamali na wadau mbalimbali wa lishe nchini.

Amesema kupitia mafunzo hayo amepata uelewa wa kina kuhusu namna sahihi ya kuandaa unga mchanganyiko, kuzingatia usafi wa mazingira ya uzalishaji, usalama na usafi wa vifaa vinavyotumika pamoja na mbinu bora za kuhakikisha bidhaa inayozalishwa ni salama kwa matumizi ya watoto.

“Maandalizi ya unga niliyokuwa nikiyafanya kabla ya mafunzo haya yana tofauti kubwa na yale niliyojifunza. Maarifa haya yatanisaidia kuboresha zaidi ubora wa unga ninaozalisha kwa ajili ya watoto,” amesema Mgaya.

TFNC inaendelea kutoa mafunzo mbalimbali kwa wadau wa lishe, wajasiriamali na wananchi kwa ujumla ili kuongeza uelewa kuhusu uandaaji wa vyakula bora na salama vinavyochangia kuboresha hali ya lishe nchini.





Leo Tarehe 03 Juni 2026,  Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC), imetembelewa na wageni kutoka Shirika la Mpango w...
03/06/2026

Leo Tarehe 03 Juni 2026, Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC), imetembelewa na wageni kutoka Shirika la Mpango wa Chakula Duniani (WFP), na kujadili masuala mbalimbali ikiwemo namna ya kuimarisha ushirikiano katika utekelezaji wa afua za urutubishaji wa vyakula nchini, ili kuongeza upatikanaji na matumizi ya vyakula vilivyorutubishwa, na hivyo kuboresha hali ya lishe na afya ya jamii.

Aidha, wajumbe hao walipata fursa ya kutembelea maabara ya Taasisi ya Chakula na Lishe iliyopo Mikocheni jijini Dar es Salaam na kujionea uwezo wake katika shughuli za uchunguzi na uchambuzi wa ubora na usalama wa vyakula, pamoja na tathmini ya viashiria mbalimbali vya lishe.





K**a wewe ni mjasiriamali  unayesindika unga kwa ajili ya chakula cha watoto wenye umri miezi sita na kuendelea, Hii si ...
01/06/2026

K**a wewe ni mjasiriamali unayesindika unga kwa ajili ya chakula cha watoto wenye umri miezi sita na kuendelea, Hii si ya Kukosa

Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC) imeandaa mafunzo ya muda mfupi yatakayo kusaidia kupata ujuzi wa kitaalamu katika kuongeza thamani bidhaa unayoizalisha. Mafunzo yatafanyika tatehe 25 - 26 Juni, 2026 katika ofisi za TFNC Mikocheni, Mtaa wa Sembeti.

Ada ya mafunzo ni Tsh. 160,000 tu. Jisajili sasa kwa kuskani QR kodi hapo kwenye tangazo ama tembelea:
https://www.tfnc.go.tz/announcements/kozi

Kwa maswali zaidi piga simu namba: 0681810080 au 0755249143

Address

Ilala

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 17:00

Telephone

0658990996

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when TFNC Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category