Mbalizi Hospital- Ifisi

Mbalizi Hospital- Ifisi A multi specialty Hospital providing quality health care & a wide range of medical services > Preventive care, Diagnosis, Treatment & Follow-Up Care.

RATIBA ZA MADAKTARI NDANI YA HOSPITALI.
17/06/2026

RATIBA ZA MADAKTARI NDANI YA HOSPITALI.

HERI YA SIKU YA MTOTO WA AFRIKA."Kulinda Afya ya Mtoto Leo, Ndio Kujenga Kesho ya Afrika. Hospitali ya Mbalizi-Ifisi Tun...
16/06/2026

HERI YA SIKU YA MTOTO WA AFRIKA.

"Kulinda Afya ya Mtoto Leo, Ndio Kujenga Kesho ya Afrika. Hospitali ya Mbalizi-Ifisi Tunajali Ustawi na Ukuaji Salama wa Mtoto Wako."

Ijali Afya ya Mwanao kwa kumfikisha Hospitalini pale unapohisi ana dalili za kuumwa.

TUNAMTUMIKIA MUNGU NA KUWAHUDUMIA WATU.
16/06/2026

TUNAMTUMIKIA MUNGU NA KUWAHUDUMIA WATU.

KARIBU KWA HUDUMA BORA ZA ULTRASOUND
16/06/2026

KARIBU KWA HUDUMA BORA ZA ULTRASOUND

KARIBU HOSPITALI YA MBALIZI-IFISI KWA HUDUMA BORA ZA VIPIMO NA MATIBABU.
15/06/2026

KARIBU HOSPITALI YA MBALIZI-IFISI KWA HUDUMA BORA ZA VIPIMO NA MATIBABU.

KUTOKA NADHARIA HADI VITENDO: HOSPITALI YA MBALIZI-IFISI YAFUNGUA MILANGO YA KITAALUMA KWA WANAFUNZI WA MUST! 🎓💼Hospital...
15/06/2026

KUTOKA NADHARIA HADI VITENDO: HOSPITALI YA MBALIZI-IFISI YAFUNGUA MILANGO YA KITAALUMA KWA WANAFUNZI WA MUST! 🎓💼

Hospitali ya Mbalizi-Ifisi inatambua mchango mkubwa wa sekta ya afya katika kukuza elimu na weledi wa vitendo kwa wataalamu wetu wajao nchini.

Mapema leo tarehe 15/06/2026 tulipata heshima ya kuwakaribisha wanafunzi wa Mwaka wa pili kutoka Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia Mbeya (MUST), wanaosomea fani ya Business Administration in Marketing and Entrepreneurship.

Wanafunzi hawa walipata fursa ya kujifunza kwa kina na kwa vitendo mifumo ya usimamizi na menejimenti ya masoko katika sekta ya afya (Hospital Marketing Management) kutoka kwa Katibu wa Afya wa Hospitali Bi. Faustina Mahenge. Kupitia darasa hili la vitendo, vijana hawa wamejionea jinsi misingi ya kibiashara, ujasiriamali, na huduma bora kwa wateja zinavyounganishwa ili kutoa huduma bora na za uhakika kwa jamii yetu.

Pia walifanikiwa kutembelea Idara Mbalimbali ikiwemo Idara ya Huduma kwa Wateja, Kitengo cha Habari na Mawasiliano, Idara ya Mapokezi na Idara ya Magonjwa ya Nje (OPD) na kujionea namna vitengo hivyo vinavyowahudumia wateja.

Mafunzo hayo yalihudhuriwa na Afisa Mdhibiti Ubora wa Hospitali Ndg. Nestory Bujiku, Mkuu wa Kitengo cha Huduma kwa Wateja Ndg. Albert Macha na Afisa Habari wa Hospitali Ndg. Sadick Issa.

Sisi k**a Hospitali ya Mbalizi-Ifisi, tunaamini katika malezi ya kitaaluma na kuwajengea uwezo vijana ili kuandaa nguvu kazi thabiti na yenye ubunifu kwa taifa letu la kesho.

Tunawashukuru viongozi na wanafunzi wa kwa kuchagua kujifunza nasi!

04/06/2026
Karibu Hospitali ya Mbalizi-Ifisi ukutane na Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Wanawake na Uzazi (Gynaecologist) kwa Changam...
03/06/2026

Karibu Hospitali ya Mbalizi-Ifisi ukutane na Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Wanawake na Uzazi (Gynaecologist) kwa Changamoto za Kutokushika Ujauzito.

Habari..🤗Ni Jumatatu mpya ya mwezi Juni, Karibu Hospitali ya Mbalizi-Ifisi kwa Huduma bora za Vipimo na Matibabu ya Kiaf...
01/06/2026

Habari..🤗

Ni Jumatatu mpya ya mwezi Juni, Karibu Hospitali ya Mbalizi-Ifisi kwa Huduma bora za Vipimo na Matibabu ya Kiafya.

"Tunamtumikia Mungu na Kuwahudumia Watu"

Mapema leo tarehe 29/05/2026 Wauguzi wa Hospitali ya Mbalizi Hospitali-Ifisi walikuwa ni miongoni mwa Wauguzi wa ndani y...
29/05/2026

Mapema leo tarehe 29/05/2026 Wauguzi wa Hospitali ya Mbalizi Hospitali-Ifisi walikuwa ni miongoni mwa Wauguzi wa ndani ya Mkoa wa Mbeya ambao wameshiriki maadhimisho ya Siku ya Wauguzi Duniani kimkoa ambayo yamefanyika katika Viwanja vya stendi ya Mbalizi.

Hafla hiyo ilitanguliwa na uwepo wa matukio mbalimbali ikiwemo wauguzi kufanya matendo ya Huruma katika Hospitali ya Mbalizi-Ifisi, Maandamano ya Amani kuelekea Stendi ya Mbalizi, Kiapo cha wauguzi waliosajiliwa pamoja na burudani mbalimbali.

Maadhimisho hayo yalihudhuliwa na Viongozi mbalimbali wakiwemo Mganga Mkuu Mkoa wa Mbeya ambaye alimuwakilisha Mkuu wa Mkoa Ndg. Beno Malisa k**a Mgeni Rasmi, Viongozi mbalimbali kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya, Wadau mbalimbali, Wauguzi na wananchi.

Ikumbukwe kwamba maadhimisho ya kitaifa ya siku ya Wauguzi yalifanyika tarehe 12/05/2026 mkoani Arusha, Hivyo siku ya leo ilikuwa ni kilele kwa wilaya zote za mkoa wa Mbeya.

Address

P. O. BOX 6117
Mbeya
53208

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mbalizi Hospital- Ifisi posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share

Category