The Cotex Medicine

The Cotex Medicine Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from The Cotex Medicine, Medical Center, thecotexmedicine@gmail. com, Morogoro.

The Cotex Medicine (the centre for Cure Coaching and Rehabilitation) ni kituo kinachotoa ushauri, usimamizi na mapendekezo juu za afya za wagonjwa wa moyo, presha na matatizo mengine ya kiafya.

*Dawa Si Kila Kitu Kwenye Matibabu,Dawa Ni Sehemu Ya Matibabu.* Dawa si kila kitu kwenye Matibabu,dawa ni sehemu ya Mati...
23/04/2023

*Dawa Si Kila Kitu Kwenye Matibabu,Dawa Ni Sehemu Ya Matibabu.*

Dawa si kila kitu kwenye Matibabu,dawa ni sehemu ya Matibabu.
Usishikirie na kuikumbatia dawa usiku na mchana na kuacha kufuata utaratibu sahihi wa kula na kunywa kuendana na hali yako.

Mara nyingi Magonjwa yanayochangiwa na mfumo wa chakula,yanahitaji dawa na yanahitaji pia uangalifu mzuri pindi unatumia hiyo dawa.

Kufuata utaratibu sahihi wa kula na kunywa wakati wa kutumia dawa ina faida nyingi, ikiwa ni pamoja na:

*1.Kuhakikisha ufanisi wa dawa:*

Kufuata maagizo ya daktari wako juu ya jinsi ya kula na kunywa wakati unatumia dawa husaidia kuhakikisha kuwa unapata faida kamili ya matibabu yako. Hii ina maanisha kuwa dawa ina nafasi ya kufanya kazi vizuri zaidi ikiwa ulaji wako utaendana na hali yako.

*2.Kuongeza uwezekano wa dawa kukupatia matokeo:*

Kufuata maagizo ya daktari wako kwenye ulaji kutakuepusha na vyakula ambavyo haviendani na dawa unayotumia na ambavyo vinaweza kupunguza ufanisi wa dawa au kufanya dawa isifanye kazi kabisaa.

*3. Kuongeza uhakika wa matibabu:*

Kufuata utaratibu sahihi wa kula na kunywa wakati wa kutumia dawa husaidia kuongeza uhakika wa matibabu yako na kurahisisha safari yako ya kupona.

*4. Kukuepusha na upoteza pesa:*

Kufuata maagizo ya daktari wako kunaweza kusaidia kuzuia upotevu wa pesa.Hii hutokea pale ambapo mtu ametumia dawa bila kufuata utaratibu sahihi wa kula na kunywa na hatimae dawa kutokumpatia matokeo sahihi.

*5. Kupunguza hatari ya kurudia matibabu:*

Kufuata utaratibu sahihi wa kula na kunywa wakati wa kutumia dawa kunaweza kupunguza hatari ya kurudia matibabu. Hii inamaanisha kuwa unapunguza hatari ya kusumbuliwa na tatizo lako la kiafya tena baada ya kupona.

Kwa ujumla, kufuata utaratibu sahihi wa kula na kunywa wakati wa kutumia dawa ni muhimu sana kwa afya yako na usalama wa matibabu yako. Ni muhimu kuzingatia maagizo ya daktari wako ili kuhakikisha kuwa unapata faida kamili ya matibabu yako.

Call/sms/WhatsApp
0678640098

23/09/2022

Jizoeshe Utaratibu Huu, Utaratibu Huu Utakusaidia Kupunguza Uzito Mkubwa/Kilo nyingi/Kitambi/Obese.

⤵️⤵️⤵️

➡️Jiwekee utaratibu wa kuruka kamba 500 hadi 600 kwa siku.

➡️Achana na vitu vyenye kuandaliwa kwa mafuta au sukari nyingi k**a maandazi,vitumbua au chapati.Badala yake tumia chai ya kijani au maziwa yasiyo na mafuta (skim milk/fat free milk) na ulaji wa vyakula vilivyoandaliwa kwa kuchemshwa au kuokwa k**a ndizi za kuchemsha au magimbi.

➡️ Asubuhi push up 15 hadi 20 na jioni pia

➡️Kula matunda na mboga mboga zaidi.

➡️Shughulisha mwili wako kwa kutembea hatua 500 au zaidi.

➡️ Punguza matumizi na ulaji wa vyakula vya wanga, punguza ulaji wa ugali wali viazi ndizi mihogo tambi n.k.Jazia mlo wako kwa kula mboga mboga na matunda zaidi,mboga zaidi k**a maharage kunde au samaki.

➡️Ikiwa we ni mpenzi wa supu,tumia supu itokayo na vyanzo vya baharini k**a supu ya samaki n.k

➡️Tumia lita moja ya maji kila asubuhi,maji ambayo umeweka ndimu kidogo au umekamulia limao.

➡️Kula mlo wako wa usiku kwa utofauti wa masaa 4 hadi 5 kabla ya kulala na ikiwa kanuni hii itakuwa ngumu kuifikia kula matunda na mboga mboga k**a mlo wako wa siku muda wowote kabla ya kulala.

➡️ Epuka matumizi ya pombe,sigara,soft drinks,kahawa/chai ya rangi n.k

➡️Pata wasaa mzuri wa kulala na kupumzika.

Note:

Ukitaka kubadilika,yakupasa ubadilishe utaratibu wako wa awali na uanze utaratibu mpya.Hakuna kazi rahisi kwenye uwanja wa vita.

Usiseme huoni mabadiliko huku bado hujaweza kuacha Yale yaliyokufanya uwe na kilo nyingi au uzito mkubwa.

For more clarification,

Nutr Sood
Call 0678640098

Address

Thecotexmedicine@gmail. Com
Morogoro

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when The Cotex Medicine posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to The Cotex Medicine:

Shortcuts

Share

Category