Dr Festo Mnyiriri Babu

Dr Festo Mnyiriri Babu Informations about health services Huduma za Afya ya mama na mtoto ushauri wa kiafya elimu ya Afya n.k

Mmelala...!? Sasa ngoja leo niwasanue...hivi mnajua ukifanya mambo yetu yale kwa njia ya mdomo..kesho yake ukienda hospi...
10/12/2023

Mmelala...!? Sasa ngoja leo niwasanue...hivi mnajua ukifanya mambo yetu yale kwa njia ya mdomo..kesho yake ukienda hospitali daktari akiangalia mdomo wako anajua kwamba huyu mama jana kalamba koni..ukilamba koni huwa inaacha alama mdomoni kwenye kaakaa laini..alama hiyo kwa kitaalam inaitwa Palatal Petechiae....kwa sasa tafiti zinaonyesha kwamba kwa baadhi ya maeneo, ngono kwa njia ya mdomo inaongoza kusababisha kansa ya koo kuliko uvutaji sigara na pombe.... mimi sijawakataza lakini....!!

Umewahi kufanyiwa ultrasound ya hivi..?!Mara nyingi ukienda hospital ukaandikiwa ultrasound huwa wanafanya tumboni kwa n...
14/10/2023

Umewahi kufanyiwa ultrasound ya hivi..?!

Mara nyingi ukienda hospital ukaandikiwa ultrasound huwa wanafanya tumboni kwa nje.

Sasa wakati mwingine ultrasound inaweza kufanyika kupitia ukeni yaani wanaingiza kile kidude k**a kirungu kwa bibi.

Hii inafanyika mtaalamu au daktari anapokuwa anataka kuona kwa karibu shingo ya kizazi, mfuko wa uzazi na o***y.

Inafanyika daktari anapokuwa anataka kuona mahali kitanzi kilipo, kuangalia ukubwa wa uterus, kuta zake zikoje, kujua umri wa mimba, kupima k**a mlango wa kizazi umelegea na mambo mengine...

Vipi umewahi kufanyiwa..!?

MJUKUU wangu k**a UNAHITAJI huduma hii nitafute tuuu 😀😀😀

NJIA 3 ZA KUTAMBUA JINSIA YA MTOTO AKIWA TUMBONI..Jinsia ya mtoto kwa mama au familia kwa ujumla hua ni suprise kutokana...
02/10/2023

NJIA 3 ZA KUTAMBUA JINSIA YA MTOTO AKIWA TUMBONI..

Jinsia ya mtoto kwa mama au familia kwa ujumla hua ni suprise kutokana na kwamba hua ni jambo lilijificha kidogo..

Kwa kifupi kabisa jinsia ya mtoto huanza kutengenezwa wiki ya saba ya ujau*ito lakini hua ni vigumu kabisa hata kitaalam kuweza kufahamu jinsia kwa kipindi hicho.

Kutokana na maendeleo ya teknolojia kuna aina kuu 3 ambazo mama anaweza kufahamu jinsia ya mtoto wake..

1. ULTRASOUND:

Njia hii ni njia ambayo mama huchunguzwa kwa kutumia ultrasound na kitaalamu jinsia huweza kuonekana vizuri kuanzia wiki ya 18 (miezi minne na wiki mbili na kuendelea ).

Hiii hutegemea na mtoto kalalaje hivyo kaka ukifanyiwa utrasound na ukaambiwa jinsia haionekani vizuri hunabudi kusubiri na kufanyiwa ultrasound kwa wakati mwingine kwa sababu mkao wa mtoto huathiri muonekano wa jinsia.

Siku zote njia hii inategemea na msomaji wa ultrasound (uzoefu wake katika kutambua jinsia)

2. AMNIOCENTESIS

Njia hii kwa nchi zetu za kiafrika bado haijaanza kutumika kwa kiasi kikubwa lakini ni kwamba njia hii huusishwa na kuchukuliwa kwa maji yaiyomo ndani ya mfuko wa uzazi (amniotic fluid)maji hayo huchambuliwa na kuweza kufahamika jinsia ya mtoto

3. Noninvasive prenatal testing (NIPT).

Hii pia ni njia ya kutambua jinsia ya mtoto lakini pia kwa hapa nchini bado haijaanza kutumika.

Ambapo mama huchukuliwa damu na damu hiyo huweza kuchunguzwa kitaalamu na kuweza kubaini jinsia ya mtoto aliyenaye...
-

Ila mtaani kwetu kuna Wazoefu wanaamini kuwa endapo utakuwa umebeba u*ito mdogo tumboni na tumbo dogo mtoto atakuwa ni wa kiume.

Mara wengine msitali ule wa kwenye tumbo😀😀😀😀😀

Kitaalamu , hakuna uhusiano wowote kwa size au muonekano wa tumbo Na jinsia ya Mtoto🤝 .

HUU NDIO UKUU WA MUNGU WAJUKUU ZANGUHuu ndio muujiza... hawa ndio mapacha wenye u*ito mdogo zaidi kuishi..wakati wanazal...
19/09/2023

HUU NDIO UKUU WA MUNGU WAJUKUU ZANGU

Huu ndio muujiza... hawa ndio mapacha wenye u*ito mdogo zaidi kuishi..wakati wanazaliwa u*ito wao wote wawili ulikuwa haufiki kilo 1....mmoja alikuwa na gram 340 na mwingine gram 425..walikaa ICU ya vichanga siku 138..Mungu kawatendea muujiza kwa sasa wako hivi...!

Ukifanyiwa OP vizuri, hata kovu halionekani kiurahisi. Hii style hushonwa KWA technic ya vertical Siku ya kutoa u*i unak...
25/08/2023

Ukifanyiwa OP vizuri, hata kovu halionekani kiurahisi. Hii style hushonwa KWA technic ya vertical

Siku ya kutoa u*i unakataa fundo upande mmoja na kuuvuta upande wa pili unatoka u*i woote tena bila maumivu

Hebu niambie kwenye comment wewe ulishonwa vipi Mjukuu WANGU na je mshono Unaonekana ?

Mungu awasaidie wajawazito wote mjifungue salama na mpakate watoto wenu

Nyanya zina kiwango kikubwa cha Vitamini C  na virutubisho vingine ambavyo hufanya kazi ya kusafisha mwili na kutoa sumu...
20/04/2023

Nyanya zina kiwango kikubwa cha Vitamini C na virutubisho vingine ambavyo hufanya kazi ya kusafisha mwili na kutoa sumu pia.

Kutokana na virutubisho hivyo nyanya husaidia kuharibu viini (free radicals) ambavyo hupelekea kutokea kwa saratani.

Pia kwa ambao wanapata MICHIRIZI KWENYE NGOZI ZAO, fanya hivi 👇🏾

Nyanya zina phytochemicals , polyphenols na carotenoids , hivi vyote huboresha muonekano na afya ya ngozi yako
Kata nyanya kipande , na usugulie kwenye eneo lenye michirizi
Acha pakauke kwa muda wa kutosha ili ngozi yako ifyonze vizuri
Osha eneo lililoathirika kwa maji ya vuguvugu
Fanya hivo kila siku na utapata matokeo mazuri baada ya mwezi mmoja.

-

Umejifunza kitu, Save post hii Itakusaidia kwa Matumizi ya Baadae,

Pia Usisahau kutufollow kupata update zaidi kuhusiana Na Vyakula tiba Na Afya ya Uzazi kwa ujumla.

Kwa msaada wa haraka wa changamoto zote za Afya ya Uzazi kwa Mwanamke,

Kunenepa Sana na kubadilika kimuonekano wakati wa ujau*ito ni Hali ya kawaida kumkumba Mwanamke, sio suala la kutaka au ...
09/04/2023

Kunenepa Sana na kubadilika kimuonekano wakati wa ujau*ito ni Hali ya kawaida kumkumba Mwanamke, sio suala la kutaka au kutotaka,

Hiyo Hali ya Mabadiliko ya homoni, hasa Growth hormone, na Estrogen. Hakuna anayetaka awe pua kubwa, au sura Pana tofauti na mwanzo😅.

Unakumbuka Nini baada ya kubeba ujau*ito, ulinenepa pua, au mdomo 😄

USHAURI KWA WANAUME WENZANGU KUHUSU WAKE ZAO WAJAWAZITO... Mimi ni mwanaume, lakini leo nataka tujadili kuhusu MIMBA. Je...
08/04/2023

USHAURI KWA WANAUME WENZANGU KUHUSU
WAKE ZAO WAJAWAZITO...

Mimi ni mwanaume, lakini leo nataka tujadili
kuhusu MIMBA.

Je! unajua kuwa mambo fulani unayomfanyia mkeo akiwa mjamzito yanachangia hali nzuri/mbaya ya afya ya mama na mtoto ambaye hajazaliwa?

Sikiliza, huwa inanisumbua sana ninapoona wanaume wanashindwa kuwajali wake zao wajawazito au kushindwa kuzoea mabadiliko fulani ya muda!!!

Ni miezi 9 tu, sio milele. Mimba hainunuliwi sokoni, wala sio App iliyodownlodiwa mtandaoni. Ni mbegu iliyopandwa na sisi wanaume na ikaota. Inabidi kuwe na mtoaji wa mbegu hiyo wakati inakua, na wanawake wamepewa jukumu la kuibeba.

Mimba ni maandalizi ya kumkaribisha Mgeni mpya kwenye familia. Mimba ni safari ya furaha..

Wanawake wametofautiana kwenye mabadiliko ya mwili. Ingawa Mimba huwafanya wanawake kufanya mambo fulani kwa pamoja.

■ Anaugua mara kwa mara
■ Anatamani kula vitu visivyofikirika k**a, udongo, mkaaa au chai iliyotiwa ndimu.
■ Anakuwa mvivu kukuandalia chakula
■Mara moja moja atataka kunyoosha miguu yake kwenye mapaja yako. Tafadhali msamehe... kubeba mtoto si rahisi.

Nusu ya kwanza ya safari inaweza kuwa ya kuudhi sana. K**a nilivyosema, wanawake hutofautiana wakati wa ujau*ito.

*😩Wengine wako busy kutapika.
*😴Wengine hulala k**a jani la maji, hulala popote hata jikoni.
*😤Wengine hushikwa na homa za mara kwa mara.
*😒Wengine wanaonekana wanyonge na wamepauka k**a poda ya Jonson.
*😱Wengine huongezeka u*ito.
*😫Wengine wanazunguka na leso Nyeupe ya kutemea mate.

HAYA YOTE BADO NI KAZI YETU.....

Tafadhali vumilia hii, ina matokeo mazuri baadaye.

Kuna wakati mambo yao yanaudhi, unapaswa kuvumilia. Lakini mimi nachoka sana ninapoona wanaume k**a mimi wakiwatelekeza wake zao wajawazito. Lazima niseme, sio safari rahisi kwa wote.

Nusu safari ya mwisho ni wakati tunatakiwa kuwa na subira zaidi, upendo, uvumilivu na kuelewa.

KUMBUKA...

1) Siku zote angalia miguu ya mkeo wakati wa ujau*ito, inavimba mara kwa mara. Tafadhali mpe beseni la maji ili aloweke mguu wake mara moja baada ya muda, ni moja ya tiba bora zaidi ambayo wanawake hufurahia wakati wa ujau*ito.

2) Muulize mara kwa mara jinsi anavyohisi na jinsi anavyomsikia mtoto. Yeye ndiye mbebaji kwa hiyo anazijua harakati zake.

3) Mwambie jinsi anavyoonekana mrembo wakati wa ujau*ito k.m

“Honey ona jinsi mimba inavyokupendeza, nitakuwa nakupa mimba kila mwezi "

au

“ni mtoto wangu anakufanya uwe mzuri namna hii kupita kawaida".

4) Usikasirike k**a atawahi kukuamsha asubuhi ili kumkanda miguu. Tunatakiwa kuhisi kidogo usumbufu na maumivu yake. Hapaswi kuhangaika peke yake, ni mtoto wetu, tunahitaji kusumbuka pamoja. (Simaanishi kubeba mimba kimwili).

5) Hakuna kitabu cha sheria kilichozuia ngono wakati wa ujau*ito, kwa kifupi ni nzuri na bora sana .... fanya hivyo, kijana endelea na kazi inayolet ujau*ito.

6) Usione aibu kumtoa out. Mtoe out mara moja moja hadi kwenye sehemu mlizokuwa mnaenda pamoja....

Natoa wito kwa wanaume wote kuwa karibu na wenzi wao wakati wa ujau*ito kwani hiyo ni moja ya nyakati anazokuhitaji sana.

Pongezi kubwa kwa wanaume wenzangu wote wanaosimama kikamilifu na wake zao wakati wa ujau*ito.

Mungu awabariki wote....

Mama K ongezeni damu 😋Mchanganyiko wa Beetroot tikit na embe na tangawiz …. K**a unapungufu wa damu iyo juice ukinywa we...
08/04/2023

Mama K ongezeni damu 😋Mchanganyiko wa Beetroot tikit na embe na tangawiz …. K**a unapungufu wa damu iyo juice ukinywa week tu kapime utakuja kunishukuru.

Umejifunza kitu, Save post hii Itakusaidia kwa Matumizi ya Baadae,

Mtag Mwanamke yeyote aje ajifunze kitu leo.

Ni vyema kuchelewesha mtoto kuoga kwa mara ya kwanza hadi saa 24 baada ya kuzaliwa au kungoja angalau yapite masaa 6 iki...
07/04/2023

Ni vyema kuchelewesha mtoto kuoga kwa mara ya kwanza hadi saa 24 baada ya kuzaliwa au kungoja angalau yapite masaa 6 ikiwa siku nzima haiwezekani. Kwa kuchelewesha kuoga mara ya kwanza, unaruhusu vernix kuendelea kufanya kazi k**a chandarua cha usalama kwa mfumo wa kinga ya mtoto wako.

''Vernix'' ni mipako ya kinga ambayo huundwa kwenye ngozi ya mtoto pindi anapokuwa kwenye mji wa uzazi. Ni dutu nene, iliyotengenezwa kwa maji, asidi ya mafuta, na protini, na hutengeneza kizuizi cha unyevu kwa ngozi ya mtoto.

Husaidia kuleta utulivu wa viwango vya sukari kwenye damu ya mtoto mchanga ili kuzoea mazingira mapya.
-

Japo Mtaani kuna mambo😀😀, Kuna mwanamke anamsema mwanamke mwenzie kuwa Katia Aibu, kisa kajifungua mtoto Mchafu ana maukoko ya mwanaume mwili mzima😀😀👐👐,

Ana amin kwamba Na kuna hizo iman, kuwa mwanamke aki s*x akijifungua ndani ya siku chache mtoto atatoka na Maukoko yaan mashahawa ya mwanaume..

Sio kweli kabisaaaa.
S*x mnaruhusiwa kufanya ni salama kabisa k**a mimba yako haina matatizo.

Mtoto akizaliwa na hayo mafuta mafuta, kazi zake ndio hizo hapo juu.

-
Je wewe uliwahi kusikia lipi juu ya ili?! Tuambie tujifunze pamoja 😃

Vichanga walazwe njeWatoto wachanga duniani kote wanahitaji uangalizi na ulinzi wa karibu sana, ingawa kulingana na tama...
05/04/2023

Vichanga walazwe nje

Watoto wachanga duniani kote wanahitaji uangalizi na ulinzi wa karibu sana, ingawa kulingana na tamaduni mbalimbali malezi hutofautiana.

Baadhi ya nchi k**a Finland, Denmark, Norway na hata Sweden watoto wachanga huachwa walale nje ya nyumba, duka au mgahawa kwenye baridi kali huku wazazi wakiwa ndani.

Japo wengine wanaweza kuona hii k**a ukatili.

Wenyewe wanasema huu ni utamaduni wao na inaaminika kusaidia upumuaji wa mtoto, kuimarisha kinga mwili, kumfanya mtoto awe na mpangilio mzuri wa kulala na kumfanya ajitegemee zaidi.

Kwa mujibu wa ukurasa wa ITK unaeleza kuwa watoto huvalishwa na kufunikwa vizuri kisha kuwekwa kwenye kikapu chao na wakati mwingine hufunikwa kwa koti la mvua ili kuzuia uchafu kutoka nje usiwafikie.

Huku wakazi wanasema watoto hawaibwi, hivyo utamkuta mwanao pale ulipomwacha.

04/04/2023

Sasa ukisikiaga mtoto amezaliwa na mgongo wazi inakuwaga hivi..

Hapo kwenye mgongo kunaweza kuwa na uvimbe ambao wakati mwingine unakuwa na kidonda ..Hii inaweza kuambatana na kichwa kikubwa..

Huwa inatibika kwa upasuaji ingawa mtoto anaweza kubaki na ulemavu wa kudumu wa miguu hali ambayo inaweza kufanya awe anatumia wheelchair maisha yake yote..

Watoto wengine huwa wanafariki .. Tatizo hili linaweza kuzuilika kwa mama kutumia vidonge vya folic acid mwezi mmoja kabla ya ujau*ito na miezi mitatu ya mwanzo ya ujau*ito..!

-

Umejifunza kitu, Save post hii Itakusaidia kwa Matumizi ya Baadae,

Pia Usisahau kutufollow kupata update zaidi kuhusiana Na Vyakula tiba Na Afya ya Uzazi kwa ujumla.

Kwa msaada wa haraka wa changamoto zote za Afya ya Uzazi kwa Mwanamke,

NITUMIE UJUMBE in box

Address

Cheyo A
Tabora

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Dr Festo Mnyiriri Babu posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Dr Festo Mnyiriri Babu:

Shortcuts

Share

Category